Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

KUVUMMILIA KATIKA SALA!


“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumamosi, Novemba 12, 2022
Juma la 32 la Mwaka wa Kanisa

Kumbukumbu ya Mt. Josafati, Askofu na Shahidi
               
3Yn 1:5-8;
Zab 111:1-6;
Lk 18:1-8


KUVUMMILIA KATIKA SALA!


Katika Injili ya leo, Yesu anatueleza habari ambayo ni kweli kabisa, kuhusu mjane ambaye hakuchoka kumsumbua kadhi dhalimu mpaka alivyompa haki yake. Kuvumilia kunalipa, na hili ni kweli kabisa na hasa kwa wale wanaomwamini Mungu. Yesu anatuelezea ni kwajinsi ghani Mungu alivyo mwepesi wakutuletea haki yake, baraka na msaada tunapo muhitaji. Lakini tunaweza kukata tamaa haraka na kuwa na mioyo hafifu katika kumwomba Baba yetu wa Mbinguni neema zake na msaada. Yesu anawapa matumaini mapya na ujasiri wafuasi wake. Katika maisha ya sasa, tunaweza kukumbana na matatizo makubwa sana na majaribu na magumu mengi lakini hatupaswi kupoteza tumaini la kumwamini Mungu. Hukumu ya mwisho itafunua kwamba haki ya Mungu itakuwa juu ya wasio haki yaliyotendwa na viumbe vyake. Yesu anamalizia kwa swali lakujiuliza sisi, je mimi na wewe tunaimani, Imani inayovumilia mpaka mwisho?

Sala: Baba Mungu, nisaidie nikuamini wewe na nikutafute wewe kila wakati katika sala bila kuchoka. Amina.


Copyright ©2013-2022 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

No comments:

Post a Comment