“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumamosi, Novemba 12, 2022
Juma la 32 la Mwaka wa Kanisa
Kumbukumbu ya Mt. Josafati, Askofu na Shahidi
3Yn 1:5-8;
Zab 111:1-6;
Lk 18:1-8
KUVUMMILIA KATIKA SALA!
Katika Injili ya leo, Yesu anatueleza habari
ambayo ni kweli kabisa, kuhusu mjane ambaye hakuchoka kumsumbua kadhi dhalimu
mpaka alivyompa haki yake. Kuvumilia kunalipa, na hili ni kweli kabisa na hasa
kwa wale wanaomwamini Mungu. Yesu anatuelezea ni kwajinsi ghani Mungu alivyo
mwepesi wakutuletea haki yake, baraka na msaada tunapo muhitaji. Lakini
tunaweza kukata tamaa haraka na kuwa na mioyo hafifu katika kumwomba Baba yetu
wa Mbinguni neema zake na msaada. Yesu anawapa matumaini mapya na ujasiri
wafuasi wake. Katika maisha ya sasa, tunaweza kukumbana na matatizo makubwa
sana na majaribu na magumu mengi lakini hatupaswi kupoteza tumaini la kumwamini
Mungu. Hukumu ya mwisho itafunua kwamba haki ya Mungu itakuwa juu ya wasio haki
yaliyotendwa na viumbe vyake. Yesu anamalizia kwa swali lakujiuliza sisi, je
mimi na wewe tunaimani, Imani inayovumilia mpaka mwisho?
Sala: Baba Mungu, nisaidie
nikuamini wewe na nikutafute wewe kila wakati katika sala bila kuchoka. Amina.
No comments:
Post a Comment