Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

FURAHA YA UPENDO WA YESU


“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumanne, Novemba 15, 2022
Juma la 33 la Mwaka wa Kanisa

Ufu 3:1-6, 14-22; 
Zab 14:2-5, 
Lk 19:1-10


FURAHA YA UPENDO WA YESU

Ni kitu ghani kilichomfanya Zakayo akafungua moyo wake, katika Injili ya leo? Ni furaha ya upendo wa Yesu. Watu walimchukia Zakayo sana na kadiri walivyo mchukia ndivyo alivyo jitenga mbali nao. Yesu anaingia katika nyumba ya Zakayo na tazama mtu aliyekuwa na moyo mgumu, unayeyuka nakuanza kuahidi maisha ya fadhila ya baadae. Je, ni kitu ghani utafanya Yesu akija kugonga katika moyo wako leo nakusema “nataka kukaa katika nyumba yako leo?” je utafurahi au utakuwa na mashaka na kudhani utadhalilika? Bwana yupo tayari daima kufanya maskani yake ndani mwetu. Je, unampa nafasi katika moyo wako na nyumbani mwako? 

Sala: Jaza nyumbani mwangu kwa uwepo wako Ee Bwana, nisaidie niweze kuonesha ukarimu na huruma kwa wote, hata kwa wale walioniumiza. Amina


Copyright ©2013-2022 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

No comments:

Post a Comment