“ASALI
ITOKAYO MWAMBANI”
Jumatatu,
Oktoba 10, 2022
Juma
la 28 la Mwaka wa Kanisa
Gal
4:22-24, 26-27, 31 - 5:1;
Zab
112:1-7;
Lk
11:29-32
UHURU
WA KWELI NDANI YA YESU!
Kama
Mt. Paulo anavyotuambia katika Somo la kwanza, tusiache kwamwe kuadhimisha
bahati kubwa ya Baraka ambayo kila mmoja anatumaini kuishiriki-baada ya kupewa
uhuru wa kweli kama watoto wa Mungu kwa njia ya Yesu Kristo. Watu wengi hawazaliwi
tu katika hali ya utumwa kwasababu ya serikali zinazo kandamiza watu kwa
ukosefu wa haki, bali wanazaliwa pia katika falsafa mbali mbali na dini ambazo,
hatujui kama zitakuwa na uhusiano wowote na Mungu wa kweli, huaribu kile
kilicho cha kweli kiasi kwamba dini huwa kama aina ya utumwa ya kuogopa zaidi
kuliko uhuru wa kutoka katika dhambi ulioletwa na Kristo. Tusichukulie uhuru
wetu kwa mizaha, bali tukumbuke kumshukuru Mungu kila siku kwa kujikuta
tumezaliwa katika hali tuliopo, au tuliofanikiwa kuingia tangu kuzaliwa.
Katika
Injili ya leo, Yesu anaposema “tazama, yupo mkuu kuliko Yona hapa” Yesu
anamuongelea nani? Anajiongelea Mwenyewe. Tumfanye Yesu awe rafiki na wa muhimu
sana katika maisha yetu. Tuweke akilini kwamba yupo nasi kila mahali, sio wakati
wa kusali tu, bali wakati unacheza, unafanya kazi, unakula, una lala. Yesu
anataka kufanya kila kitu pamoja nasi. Kadiri unavyotambua uwepo wa Yesu katika
kila jambo unalofanya katika maisha yako, ndivyo unavyokuwa katika hali ya juu
ya muunganiko wa ndani pamoja naye. Ukitambua upo na Yesu kila wakati huwezi
kumtenda jirani yako vibaya kwa jinsi yeyote ile, labda kwa kumsema vibaya au
kwa namna nyingine ile. Wayahudi wengi walikataa urafiki wake. Je, unataka
kukataa uhuru unaokuja kwasababu ya kuwa na urafiki na Yesu?
Sala:
Nakushukuru Ee Bwana, kwa uhuru tunaofurahia kama watoto wa Baba Yetu wa
Mbinguni. Amina.
Copyright
©2013-2022 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com
No comments:
Post a Comment