MASOMO
YA MISA, OKTOBA 17, 2024
ALHAMISI,
JUMA LA, 28 LA MWAKA WA KANISA
SOMO
1
Efe.
1:1, 3 – 10
Paulo,
mtume wa Kristo Yesu, kwa mapenzi ya Mungu; kwa watakatifu wanaomwamini Kristo
Yesu.
Atukuzwe
Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa Baraka zote za rohoni,
katika ulimwengu war oho, ndani yake Kristo; kama vile alivyotuchagua katika
yeye kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, ili tuwe watakatifu, watu wasio na
hatia mbele zake katika pendo. Kwa kuwa alitangulia kutuchagua, ili tufanywe
wanawe kwa njia ya Yesu Kristo, sawasawa na Uradhi wa mapenzi yake.
Na
usifiwe utukufu wa neema yake, ambayo ametuneemesha katika huyo Mpendwa. Katika
yeye huyo, kwa damu yake, tunao ukombozi wetu, masamaha ya dhambi, sawasawa na
wingi wa neema yake. Naye alituzidishia hiyo katika hekima yote na ujuzi;
akiisha kutujulisha siri ya mapenzi yake, sawasawa na Uradhi wake, alioukusudia
katika yeye huyo. Yaani, kuleta madaraka ya wakati mkamilifu atavijumlisha vitu
vyote katika Kristo, vitu vya mbinguni na vitu vya duniani pia.
Neno
la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO
WA KATIKATI
Zab.
98:1 – 6 (K) 2
(K)
Bwana ameufunua wokovu wake.
Mwimbieni
Bwana wimbo mpya,
Kwa
maana ametenda mambo ya ajabu,
Mkono
wa kuume wake mwenyewe,
Mkono
wake mtakatifu umemtendea wokovu. (K)
Bwana
ameufunua wokovu wake,
Machoni
pa mataifa ameidhihirisha haki yake.
Amezikumbuka
rehema zake,
Na
uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli. (K)
Miisho
yote ya dunia imeuona
Wokovu
wa Mungu wetu.
Mshangilieni
Bwana, nchi yote,
Inueni
sauti, imbeni kwa furaha, imbeni zaburi. (K)
Mwimbieni
Bwana zaburi kwa kinubi,
Kwa
kinubi na sauti ya zaburi.
Kwa
panda na sauti ya baragumu,
Shangilieni
mbele za Mfalme, Bwana. (K)
SHANGILIO
Zab.
119:105
Aleluya,
aleluya,
Neno
lako ni taa ya miguu yangu, na mwanga wa njia yangu.
Aleluya.
INJILI
Lk.
11:47-54
Yesu
aliwaambia wanasheria: Ole wenu, kwa kuwa mwajenga maziara ya manabii, na baba
zenu ndio waliowaua. Basi, mwashuhudia na kuziridhia kazi za baba zenu; kwa
kuwa wao waliwaua nanyi mwawajengea maziara.
Na
kwa sababu hiyo hekima ya Mungu ilisema, Tazama, nitatuma kwao manabii na
mitume, nao watawaua baadhi yao na kuwafukuza, ili kwa kizazi hiki itakwe damu
ya manabii wote, iliyomwagika tangu kupigwa msingi wa ulimwengu; tangu damu ya
Habili hata damu ya Zakaria, aliyeuawa kati ya madhabahu na hekalu. Naam,
nawaambieni ya kwamba itatakwa kwa kizazi hiki.
Ole
wenu, enyi wanasheria, kwa kuwa mmeuondoa ufunguo wa maarifa; wenyewe
hamkuingia na wale waliokuwa wakiingia mmewazuia.
Alipotoka
humo, waandishi na Mafarisayo walianza kumsonga vibaya, na kumchokoza kwa
maswali mengi, wakimvizia, ili wapate neno litokalo kinywani mwake.
Neno
la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo
Copyright
© 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture
readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by
T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible
Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki:
see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment