Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

JE TUNA UPANA WA AKILI KATIKA MAISHA YETU?



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Alhamisi, Oktoba 17, 2024
Juma la 28 la Mwaka wa Kanisa

Ef 1:1-10;
Zab 97:1-6;
Lk 11:47-54


JE TUNA UPANA WA AKILI KATIKA MAISHA YETU?


Injili ya leo inaongelea kuhusu kutokuelewana kati ya Yesu na viongozi wa dini wa wakati huo. Walimu washeria walimwelezea Mungu kama hakimu mkali sana na wakaweka sheria na miiko ambazo hazikuwa na ushusiano kabisa na amri za Mungu. Wao kwa njia ya mafundisho ya uongo waliwahukumu na kuwaua Manabii, na baadaye walitengeneza makaburi kwa heshima yao. Leo Yesu anawanyoshea kidole, kwamba wanajizuia wenyewe nakujiwia mizigo katika kuingia Ufalme wa Mungu na pia kuua hamu ya wengine ya kumtumikia Mungu.

Swali ambalo tunaweza kujiuliza wenyewe:
• Je, tuna sura ya uongo ya Mungu na tunajaribu kuiweka kwa wengine?
• Je, tuna upana mdogo wa uwelewa kama Waandishi ambao waliwapinga wengine kwasababu tu, wanafikiri tofauti na kutenda tofauti?

Sala: Bwana, naomba utupilie mbali mawazo yote mabaya na mitazamo yote mibaya inayonizuia kujikabidhi kwangu kwako, mimi na jirani yangu, nisaidie niweze kuwa na upana wa akili katika kukuelewa wewe katika jamii na jumuiya yangu. Amina.


Copyright ©2013-2024 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com


No comments:

Post a Comment