Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

KUSALI KWA IMANI!



“MBEGU ZA UZIMA”
Jumapili, Oktoba 5, 2025 
Dominika ya 27 ya Mwaka


Hab 1:2-3; 2:2-4
Zab 95: 1-2, 6-9
2 Tim 1: 6-8, 13-14
Lk 17: 5-10


KUSALI KWA IMANI!

Biblia haijasema kama Abrahamu alienda kwenye mapango kusali lakini anachukuliwa Baba wa imani: baba wa imani na mfano wa sala. Maisha Yake yanatawaliwa na sala na imani; alifanya vitu tu baada ya kusikia sauti ya Mungu; alichukua jukumu na kutekeleza na kushika njia mara baada ya kusikia neno la Bwana. Maisha Yake yanatawaliwa na mazungumzo baina Yake na Mungu. Mungu alimwambia Abram: nenda....Abram akaondoka... (Mwa 12:1,4)... " Neno la Mungu lilimjia Abram katika ndoto .....  na Abram akasema: Bwana utanipa nini Mimi?”… (Mwa 15:1,2). Bwana alimtokea katika Mamre na hapo akainamisha kichwa chake ardhini" Mwa 18:1-3). “Bwana alimjaribu Abram... Abram akajibu nipo hapa!”(Mwa 22:1) mazungumzo haya yaliijaza imani ya Abraham, yalimwandaa kupokea mapenzi ya Mungu.

Nabii Habakuki aliishi na changamato nyingi sana katika imani Yake. Ukosefu wa Haki, maovu katika jamii yanaonesha Mungu hapendezwi na haingilii kati. Habakkuki ana jaribu Kuelewa yanayotea na haogopi kuanza masungumzo na Mungu. Anathubutu kumuuliza Mungu kwa ujasiri kwamba anapingana naye, kwamba haelewi kukaa kwake kimya bila kutenda kitu dhidi ya maovu, anamkumbusha juu ya ukimya wake na kutokufanya kitu; anathubutu kumwambia atoe hesabu ya njia zake juu ya kuutawala ulimwengu na matukio ya kihistoria. Baada ya kutoa malalamiko yake, na juu ya uovu wa watu, nabii anakaa kimya. Ni wakati wa Mungu kujibu. Mungu anajibu, hatoi maelezo yeyote, anadai juu ya uaminifu usio na masharti. Anajua juu ya mapungufu ya nabii na ya watu; alijua kwamba hawawezi kuelewa sababu ya ukimya wake wakutokufanya kitu. Badala yake anatoa uhakika kwamba kilichosemwa leo siku moja kitaeleweka kwa wote. 

Katika somo la pili mtume Paulo pia anaongelea kuhusu imani. Timoteo anaongelea kuhusu kuwa na imani, kwa njia yake kueneza matendo ya huruma. Mfuasi pia anaalikwa kuwa mkarimu katika Imani, zawadi ya Mungu ambayo ipo ndani yake na kwanjia ya kuwekea mikono, anasimikwa kama zawadi, aliyopokea ili aweze kuchukua kazi zake za kitume kama msaidizi wa Paulo. (2 Tim 1: 6). 

“Imani” katika uhalisia ni kujikita kwa mtu, kujikabidhi kwa mtu, uaminifu, na mshikamono unaotoka katika uaminifu huo. Ndio kusema, mitume hawamuombi Yesu kuongeza uelewa wao au akili zao kuhusu mambo. Wanamuomba Yesu aongeze uaminifu wao kwake. Yesu bila kujibu moja kwa moja sala yao, anatumia njia nyingine na anatumia taswira ya picha kuelezea hali ya juu ya Imani na umuhimu wake. Kama vile Kamba yaweza kushikilia kitu kizito kuliko kamba yenyewe, ndivyo ilivyo kwa Imani kidogo, inaweza kufanya kitu kikubwa ambacho huwezi kufikiria, kitu cha hali ya juu, kama vile kungoa mti mkubwa na kuupanda baharini. Imani, ndio kusema, kumuamini Kristo, kumkaribisha, na kumfanya atubadilishe, kumfuata mpaka mwisho kabisa, inafanya mambo ya mwanadamu yasiowezekana yawezekane katika hali zote. 

Mbegu ni kwa ajli ya kupanda, ili vitu vingine vizuri zaidi vinavyopendwa viote. Tunapo otesha mbegu ya Imani yetu, inasababisha Imani zaidi iweze kukuwa, na matendo ya Imani, ambayo ni upendo wa Mungu, haki na huruma. Kwa njia hii tunaleta upendo wa Mungu kwa wasio pendwa, nakupenda, huruma ya Mungu kwa wasio na huruma na kwa wote ambao hawajaitambua huruma ya Mungu maishani mwao. Tunafanya haki ya Mungu ikuwe katika maeneo yasio na upendo, yenye vita na dhuluma, na kwa mioyo isio na haki. Tuna sababisha Imani ikuwe kwenye mioyo ya watu ambao hawakuwa na Imani, au kwa walio poteza Imani yao kwasababu ya kuboreka na kupoteza tumaini. Kwa kupanda na kupalilia mbegu ya Imani, tunakuta na Imani yetu wenyewe inakuwa, na jukumu kama kusamehe, kila mara inamfanya mtu iwe rahisi na neema kukuwa zaidi, ni kama sehemu za kazi katika maisha yetu, kadiri tufanyavyo kazi flani ndivyo inakuwa rahisi na nyepesi katika kuitenda: mfano pia, kucheza mpira, kucheza ala za muziki, kutengeneza picha nk. Imani yetu inatosha na ni muhimu. Tuna sehemu ya kusimamia na kuwa vyote anavyotaka Mungu.

Matukio mengi katika maisha yetu yanaweza kuonekana ya kushangaza na hayafikiriki na yanatufanya tuwe na maswali kuhusu uwepo wa Mungu. Kipindi hiki Imani yetu inawekwa kwenye majaribu makubwa, na mara nyingi tunamlilia Mungu na kumuomba msaada. “Bwana sikia sala yangu” sikiliza kilio chetu”. Mungu kila wakati anasikia sauti zetu ingawaje ni vigumu kwetu kutambua sauti yake. Sala ndio inayo fungua moyo wetu, inatusaidia kuelezea mahitaji yetu, ulinzi wetu na mipango yetu na hapo kutufanya sisi tuyakaribishe mapenzi ya Mungu katika maisha yetu. Tutafute Imani iliojitosheleza na thabiti kwa Mungu kwa njia ya sala. Imani tukiwa katika mateso yetu, Imani kuona mapenzi ya Mungu yametimia katika maisha yetu. 

Sala: Bwana Yesu, ongeza Imani yetu na utufanye tuwe watumishi wako wa aminifu, ili tuendelee kufanya utume wako na kukushuhudia Wewe. Amina.


Copyright ©2013-2025 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA JUMAPILI, OKTOBA 5, 2025



MASOMO YA MISA 
JUMAPILI, OKTOBA 5, 2025
DOMINIKA YA 27 YA MWAKA


SOMO 1
Hab. 1:2 – 3; 2:2 – 4

Ee Bwana, nilie hata lini, wewe usitake kusikia? Nakulilia kwa sababu ya udhalimu, ila hutaki kuokoa. Mbona wanionyesha uovu, na kunitazamisha ukaidi? Maana uharibifu na udhalimu u mbele yangu; kuna ugomvi, na mashindano yatokea. Bwana akanijibu, akasema, Iandike njozi ukaifanye iwe wazi asana katika vibao, ili aisomaye apate kuisoma kama maji. Maana njozi hii bado ni kwa wakati ulioamriwa, inafanya haraka ili kuufikilia mwisho wake, wala haitasema uongo; ijapokawia; ingojee; kwa kuwa haina bidi kuja, haitakawia. Tazama, roho yake hujivunia, haina unyofu ndani yake; lakini mwenye haki ataishi kwa Imani yake.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 95:1 – 2, 6 – 9, (K) 7 – 8

(K) Ingekuwa heri leo tusikie sauti yake! Tusifanye migumu mioyo yetu.

Njoni tumwimbie Bwana,
Tumfanyie shangwe mwamba wa wokovu wetu.
Tuje mbele yake kwa shukrani, 
Tumfanyie shangwe kwa zaburi. (K)

Njoni, tuabudu tusujudu,
Tupige magoti mbele za Bwana aliyetuumba.
Kwa maana ndiye Mungu wetu,
Na sisi, tu watu wa malisho yake,
Na kondoo za mkono wake. (K)

Ingekuwa heri leo msikie sauti yake!
Msifanye migumu mioyo yenu;
Kama huko Meriba;
Kama siku ile ya Musa jangwani,
Hapo waliponijaribu baba zenu,
Wakanipima, wakayaona matendo yangu. (K)


SOMO 2
2Tim. 1:6 – 8; 13 – 14

Ndugu yangu, nakukumbusha, uichochee karama ya Mungu, iliyo ndani yako kwa kuwekewa mikono yangu. Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu nay a upendo nay a moyo wa kiasi. Basi usiuonee haya ushuhuda wa Bwana wetu, wal ausinionee haya mimi mfungwa wake, bali uvumilie mabaya pamoja nami kwa ajili ya Injili, kwa kadiri ya nguvu ya Mungu. Shika kielelezo cha maneno yenye uzima uliyoyasikia kwangu, katika Imani na upendo ulio katika Kristo Yesu. Ilinde ile amana nzuri kwa Roho Mtakatifu akaaye ndani yetu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


SHANGILIO
Yn. 15:15

Aleluya, aleluya,
Ninyi nimewaita rafika, 
kwa kuwa yote niliyoyasikia 
kwa baba yangu nimewaarifuni.
Aleluya!


INJILI
Lk. 17:5 – 10

Mitume walimwambia Bwana, Tuongezee Imani. Bwana akasema, Kama mngekuwa na Imani kiasi cha chembe ya haradali, mngeuambia mkuyu huu, Ng’oka, ukapandwe baharini, nao ungewatii.

Lakini, ni nani kwenu mwenye mtumwa alimaye au achungaye ng’ombe, atakayemwambia mara arudipo kutoka shambani, Njoo upesi, keti, ule chakula? Je! Hatamwambia, Nifanyie tayari chakula, nile; jifunge unitumikie, hata niishe kula na kunywa, ndipo nawe utakapokula na kunywa? Je! Atampa asante yule mtumwa; kwa sababu ameyafanya aliyoagizwa? Vivyo hivyo nanyi, mtakapokwisha kuyafanya yote mliyoagizwa, semeni, Sisi tu watumwa wasio na faida; tumefanya tu yaliyotupasa kufanya.

Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

4th OCTOBER 2025


 

FURAHA KAMILI




“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Kila siku
Jumamosi, Oktoba 4, 2025
Juma la 26 la Mwaka wa Kanisa


Bar 4: 5-12, 27-29;
Zab 69: 33-37 (R) 34;
Lk 10: 17-24.


FURAHA KAMILI

Nabii Baruku anawapa watu wa Mungu matumaini wale walio msahau Mungu wa kweli na kuchokoza hasira yake kwa kutolea sadaka miungu mingine na sio yeye. Baruku anawaalika sasa watubu sasa na kumrudia mara kumi zaidi. Na kama watafanya hivi watapokea furaha ya milele na ukombozi.

Furaha hii kamili inatoka katika Injili ambayo unaweza kuisoma katika hali tatu.

1) Furaha ya huduma: wale sabini wamerudi na kutoa taarifa ya ushindi kwa Yesu. Aliwapa mamlaka ana nguvu ya kuponya, kufukuza pepo na kuhubiri neno la Mungu, na walifanikiwa sana! Wakiwa katikati ya furaha yao kubwa, walikuwa makini kumpa Mungu utukufu. Ushindi wao ulikuwa wa kumuangamiza na kumshinda shetani. Tunaitwa kuendelea na utume huo huo.

2) Furaha ya ukombozi: Yesu anawaonya wasije wakaenda kwasababu ya ushindi wao bali wafurahi kwasababu majina yao yameandikwa mbinguni. Pamoja na muujiza wao kuwa mkubwa, bado muujiza mkubwa kuliko wote ni roho iliopotea kurudi kwa Mungu.

3) Furaha ya utawala: furaha yetu kubwa haipatikani katika huduma yetu au katika ukombozi wetu, bali kuhesabiwa katika mamlaka na utawala wa Baba yetu wa mbinguni, kwani huu ndio msingi wa huduma yetu na ukombozi. Hapa tunamuona Mungu Mwana akifurahi kwa njia ya Roho Mtakatifu kwasababu ya mapenzi ya Baba! “Baba ndivyo ilivyokupendeza kwani yalikuwa mapenzi yako”.

Sala: Bwana ninakuomba nipate furaha hiyo kwa huduma yangu na zaidi sana katika ukombozi kwa kujikabidhi katika kuyafanya mapenzi yako. Amina
  
Copyright ©2013-2025 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, OKTOBA 4, 2025

 



MASOMO YA MISA, OKTOBA 4, 2025
JUMAMOSI, JUMA LA 26 LA MWAKA
________
SOMO 1
Bar. 4:5-12, 27-29

Jipeni moyo, watu wangu, Israeli mnaokumbukwa! Mliuzwa kwa mataifa, lakini hamkuangamia. Kwa kuwa mlimtia Mungu ghadhabu mlitolewa kwa adui zenu; Mlimwasi Yeye aliyewaumba, mkitoa sadaka kwa pepo, si kwa Mungu; Mlimsahau Mungu wa milele aliyewalea, na Yerusalemu, mama yenu. Huyu mama aliiona ghadhabu ya Mungu iliyokuja juu yenu, akasema:

Enyi wa Sayuni, sikilizeni! Mungu ameleta juu yangu huzuni kubwa. Nimeuona utumwa wa wanangu ambao Aliye wa Milele amewapatiliza. Kwa furaha naliwalea; Bali kwa kilio na maombolezo naliwaaga. Asisimange juu yangu mtu yeyote, mimi niliye mjane na kuachwa nimeachwa ukiwa, kwa kuwa walikengeuka na kuiacha sharia ya Mungu.

Jipeni moyo, wanangu, mlilieni Mungu! Maana Yeye aliyewapatiliza mambo haya atawakumbuka. Kama ilivyokuwa nia yenu kumwasi Mungu, rudini sasa, mtafuteni mara kumi Zaidi; maana Yeye aliyeyaleta mapigo haya juu yenu atawarudishia furaha ya milele pamoja na wokovu wenu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab. 69: 32-36  (K) 33

(K) Bwana huwasikia wahitaji.

Walioonewa watakapoona watafurahi;
Enyi mmtafutao Mungu, mioyo yenu ihuishwe.
Kwa kuwa Bwana huwasikia wahitaji,
Wala hawadharau wafunga wake.
Mbingu na nchi zimsifu,
Bahari na vyote viendavyo ndani yake. (K)

Maana Mungu ataiokoa Sayuni,
Na kuijenga miji ya Yuda,
Na watu watakaa ndani yake na kuimiliki.
Wazao wa watumishi wake watairithi,
Nao walipendao jina lake watakaa humo. (K)


SHANGILIO
Yn. 14:23

Aleluya, aleluya,
Mtu akinipenda, atalishika neno langu, na Baba yangu atampenda, na sisi tutakuja kwake.
Aleluya.


INJILI
Lk. 10:17-24

Wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako. Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme. Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru. Lakini, msifurahi kwa vile pepo wanavyowatii; bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.

Saa ile ile alishangilia kwa Roho Mtakatifu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya umewaficha wenye hekima na akili; umewafunulia watoto wachanga; Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyokupendeza. Akasema, Nimekabidhiwa vyote na Baba yangu, wala hakuna amjuaye Mwana ila Baba; wala hakuna amjuaye Baba ila Mwana, na yeyote ambaye Mwana apenda kumfunulia.

Akawageukia wanafunzi wake, akasema nao kwa faragha, Heri macho yaonayo mnayoyaona ninyi. Kwa kuwa nawaambia ya kwamba manabii wengi na wafalme walitamani kuyaona mnayoyaona ninyi wasiyaone; na kuyasikia mnayoyasikia ninyi wasiyasikie.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

 ________

Copyright © 2025, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

RUDI KWA MUNGU!


Tafakari ya Kila siku
Ijumaa, Oktoba 3, 2025
Juma la 26 la Mwaka

Bar 1: 15-22;
Ps 78: 1-5, 8-9;
Lk 10: 13-16


RUDI KWA MUNGU!


Tunasikia leo maneno mazito kutoka kwa Yesu leo juu ya miji ambayo amehubiri kwa nguvu-Korazini, Bethsaida na zaidi Kapernaumu. Kama Yesu akitembelea jumuiya yetu leo atasema nini? Je atatoa onyo kama alivyofanya kwa Korazini na Bethsaida? Na je tutajibuje?

Kila sehemu alipo enda Yesu alifanya makuu kuwaonesha ni kwa jinsi ghani Mungu anawapenda. Korazini na Bethsaida walibarikiwa kwa kutembelewa na Mungu. Walisikia neno la Mungu, habari njema na kuona miujiza mikuu aliyo tenda Yesu kwa ajili yao. Lakini hawa watu waliosikia Injili hapa waliitika kwa mwaliko mdogo kabisa. Yesu anawaonya kwa kutokufanya kitu. Toba ni wito wa daima kwetu kutoka kwa Yesu na tunapaswa kuusikiliza.

Kutatokea nini tusipo sikiliza?
Kutakuwa na adhabu na hiyo adhabu haitatoka kwa Mungu bali itakuwa ni matokeo ya dhambi zetu wenyewe. Kwa mfano mtu ambaye ameshauriwa asitumie pombe, badala ya kusikiliza akadharau. Na baadae akazidiwa na pombe na kufa. Kuna mifano mingi, ambayo watu hawabadilishi mienendo yao na kujikuta wakipokea adhabu ambayo inasababishwa na matokeo ya dhambi yao wenyewe. Inatoka katika matokeo ya matendo yao wenyewe.

Toba inahitaji kubadili moyo na mwenendo wa maisha. Neno la Mungu ni uzima na lina okoa maisha yetu ya mwili na roho. Hasira ya Yesu ameilekeza kwa dhambi na yale yote yanayo tusonga tushindwe kutimiza mapenzi ya Mungu. Kwahiyo kwa nini tusibadilike na kuanza maisha mapya ya ukweli na mazuri? Kwa mapendo anatuita sisi tutembee katika njia ya haki, ukweli na uhuru, neema na utakatifu. Je, unapokea neno lake kwa Imani na utii au kwa mashaka na shingo upande?

Sala: Mungu mkuu na mtukufu, angaza giza la moyo wangu, utupe sisi Imani ya kweli, matumaini na mapendo kamili. Yesu, nakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2023 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, OKTOBA 3, 2025

 


MASOMO YA MISA, OKTOBA 3, 2025
IJUMAA, JUMA LA 26 LA MWAKA

 

SOMO 1

Bar 1:15-22

 

Kwa Bwana Mungu wetu, haki; lakini kwetu sisi haya ya uso kama hivi leo, kwa watu wa Yuda na kwa wenyeji wa Yerusalemu, na kw awafalme wetu, na kwa wakuu wetu, na kwa makuhani wetu, na kwa manabii wetu, na kwa baba zetu, kwa sababu tumetenda dhambi mbele ya Bwana. Tumemwasi, wala hatukuitii sauti ya Bwana Mungu wetu, kwenda katika sheria zake alizoziweka mbele yetu. Tangu siku Bwana aliyowatoa baba zetu katika nchi ya Misri hata leo tumemwasi Bwana Mungu wetu na kutenda yasiyofaa kwa kutoisikiliza sauti yake. Kwa hiyo mapigo haya yameshikamana nasi, na ile laana ambayo Bwana alimwamuru mtumishi wake Musa, katika siku aliyowaleta baba zetu kutoka katika nchi ya Misri ili atupe nchi ijaayo maziwa na asali, kama hivi leo. Lakini hatukuisikiliza sauti ya Bwana Mungu wetu, kwa kuyafuata maneno yote ya manabii aliyotupelekea, bali tulikwenda kila mtu katika mawazo ya moyo wake mbaya, kutumikia miungu ya kigeni na kufanya yaliyo maovu machoni pa Bwana Mungu wetu.

 

Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu

 

 

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 79:1-6, 8-9

 

(K) Utusaidie, Ee Mungu, kwa ajili ya utukufu wa jina lako.

 

Ee Mungu, mataifa wameingia katika urithi wako,

Wamelinajisi hekalu lako takatifu.

Wamefanya Yerusalemu chungu chungu.

Wameziacha maiti za watumishi wako

Ziwe chakula cha ndege wa angani.

Na miili ya watauwa wako Iwe chakula cha wanyama wa nchi. (K)

 

Wamemwaga damu yao kama maji

Pande zote za Yerusalemu,

Wala hapakuwa na mzishi.

Tumekuwa lawama kwa jirani zetu,

Mzaha na dhihaka kwao wanaotuzunguka.

Ee Bwana, hata lini? Utaona hasira milele?

Wivu wako utawaka kama moto? (K)

 

Usikumbuke juu yetu maovu ya baba zetu,

Rehema zako zije kutulaki hima.

Kwa maana tumedhilika sana. (K)

 

Ee Mungu wa wokovu wetu, utusaidie,

Kwa ajili ya utukufu wa jina lako.

Utuokoe, utughofiri dhambi zetu,

Kwa ajili ya jina lako. (K)

 

 

SHANGILIO

Yn 10:27

 

Aleluya, aleluya,

Kondoo wangu waisikia sauti yangu, nami nawajua, nao wanifuata.

Aleluya.

 

 

INJILI

Lk 10:13–16

 

Yesu aliwaambia wafuasi wake: Ole wako, Korazini! Ole wako, Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza hiyo iliyofanyika kwenu ingalifanyika katika Tiro na Sidoni, wangalitubu tangu hapo, huku wakiketi katika nguo za kigunia na majivu. Lakini, siku ya hukumu itakuwa rahisi Tiro na Sidoni kustahimili adhabu zake kuliko ninyi. Nawe Kapernaumu, je! Utakuzwa hata mbinguni? Utashushwa hata kuzimu. Awasikilizaye ninyi anisikiliza mimi, naye awakataaye ninyi anikataa mimi; naye anikataaye mimi amkataa yeye aliyenituma.

 

Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo
________

Copyright © 2025, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

3rd OCTOBER 2025


 

2nd OCTOBER 2025


 

MALAIKA –ULINZI WA MUNGU KWETU



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Alhamisi, Oktoba 2, 2025.
Juma la 26 la Mwaka

Kumbukumbu ya Malaika Walinzi

Kut 23: 20-23;
Zab 90: 1-6, 10-11;
Mt 18: 1-5, 10


MALAIKA –ULINZI WA MUNGU KWETU


Kanisa Katoliki linafundisha tunapaswa kukumbuka ni kwa jinsi ghani ilikuwa lengo la Mungu la kuwaweka malaika walinzi kwa ajili ya kuwalinda wanadamu na kuwaongoza, kwa kila mwanadamu, ili wasije wakaanguka katika hatari kubwa. Masomo yanatoa mwanga wa ujumbe huu.

Katika somo la kwanza tunasikia kwamba Waisraeli walipewa malaika wa kuwaongoza katika safari yao, na kwamba kama watamtii Mungu atawapa ushindi juu ya maadui zake. Katika somo la Injili tunajifunza kwamba watoto hawapaswi kudharauliwa au kukataliwa, wana thamani mbele ya Mungu kwani malaika wao wapo mbele za Mungu daima. Katika maisha yetu ya kila siku malaika wa Mungu huongea nasi kutuelekeza kuacha njia mbaya na kugeukia mema, au kwa kutuweka katika hali ambazo tutajifunza kuacha ubaya kwa tukio fulani au kwa njia ya dhamiri zetu lakini pia aweza kutumia watu watuambie tuache jambo fulani kuepuka ubaya, lakini daima hawaingilii uhuru kamili wa mtu. Lakini tunabarikiwa sana tunapo amua kusikiliza sauti yao ya kutuambia tuache ubaya na kujeukia mema.

Tafakari, leo, juu ya zawadi ya malaika wako mlinzi. Huyu kiumbe wa Mungu aliumbwa ili akuhudumie wewe na baadaye akufikishe Mbinguni. Ongea na malaika wako leo. Kwa kutegemea maombi ya malaika wako ruhusu huyu Malaika Mtakatifu wa Mungu azungumze na wewe kwa njia ya neema kuu.

Sala: Malaika wa Mungu mpendwa, ambaye kwa njia ya mapendo yake mimi nipo hapa, endelea kuwa nami daima, kuniangazia na kunikinga amina. Malaika wa Mungu , mniombee. Yesu nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2025 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.