Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

KUKUTANA NA MCHUNGAJI MWEMA!



“MBEGU ZA UZIMA”
Tafakari ya Pasaka
Aprili 21, 2024. 

------------------------------------------------
JUMAPILI,  DOMONIKA YA 4 YA PASAKA MWAKA B 

Somo la 1: Mdo 4:8-12 Petro akijazwa Roho Mtakatifu anasema, “uponyaji wa kiwete yule ulifanywa na Yesu mfufuka ambaye walimuua hapo kwanza.”

Wimbo wa katikati : Zab 118:1,8-9,21-23,26,28-29 Ni vyema kumtumainia Bwana kuliko kutegemea wanadamu.

Somo la 2: 1 Yn 3:1-2 Yohane anawaambia wakristo wa kipindi hicho na sisi kwamba sisi ni watoto wa Mungu tukiwa tunaishi kwa uzima wa Kimungu ambao upo ndani ya Mungu. 

Injili: Yn 10:11-18 Yesu anawambia maadui wake na sisi kwamba yeye ni Mchungaji mwema anaye wafahamu kundi lake, anampenda kila mmoja na yupo tayari kufa kwa ajili yao. 
------------------------------------------------

KUKUTANA NA MCHUNGAJI MWEMA!

Tazama ni upendo wa namna gani alionao Baba kwetu kwamba sisi tuitwe wanawake na kweli ndivyo tulivyo (Somo la 2). Kila mmoja anapaswa kutafakari juu ya maneno haya wakati maneno haya yakiwa yanazama ndani ya mioyo yetu. Yohane anaongea kuhusu wewe na mimi! Je, mimi ni mtoto wa Mungu? Ndio, hilo nimefunuliwa kweli. Uzima ulio katika maisha ya Kimungu katika Utatu Mtakatifu upo ndani yetu, ni uzima wetu pia. Uhusiano wetu huu ni sehemu ya adhimisho letu leo. 


Jumapili ya nne ya Pasaka inajulikana kama jumapili ya Mchungaji Mwema, kama Yesu anavyo jiongelea mwenyewe kuwa ni “Mchungaji mwema”. Yesu anatupa sura ya Mchungaji mwema anaye wafahamu kondoo wake: anawaita, anawalisha na kuwaongoza. Ni kwasababu ya hili Kanisa limeipendekeza kuwa siku ya kuombea miito duniani.

Yesu anaonesha wazi tofauti ya wachungaji. Tofauti anayotoa ni juu ya mchungaji yule anaye wafahamu kondoo wake na kuwajali, na wale wanaofuata tu mkumbo bila sadaka ya upendo. Yesu alitolea sadaka kamilifu kama Mchungaji wa Kimungu. Alikuwa yupo tayari kutembea nasi katika njia zote, sisi kondoo wake. Alikuwa yupo tayari kutoa sadaka ya kila kitu. Hakutaka mateso, kuonewa, kukataliwa na mambo mengine yamuondoe kutoka katika lengo lake la kuwajali na kuwatunza watu wake katika njia kamili. Inapaswa ituguse na sisi, kutufariji na kutupatia sisi ujasiri na kutambua ni kwa jinsi ghani upendo wake ulivyokuwa mkubwa kwetu. 

Wakati upendo aliotoa mmoja kwa ajili yetu ni kamili, tena wakati wa wakati mgumu, huu ni msaada mkubwa. Na upendo unaotolewa kwa mwingine kama huu unatengeneza muunganiko wa kiroho ambao ni imara kuliko matatizo tunayo weza kukutana nayo. Haijalishi ni kitu ghani kigumu kinachoweza kuja katika njia zetu, tunapaswa kutambua upendo na msaada usio na kikomo kutoka kwa Mchungaji wetu mwema. Na kama tunaweza kuona upendo huo kamili kutoka kwa wengine, tunakuwa kweli tumebarikiwa mara mbili. Katika hali nyingine Yesu anaongea kuhusu mfano wa mtu mwingine ambaye sio mchungaji mwema, ambaye anaona mbwa mwitu wakija na yeye hukimbia. Tunapaswa kuona ndani ya mtu huyu, vishawishi vyote ambavyo vyaweza kuja katika maisha yetu. Ni vigumu kubaki wakati wa nyakati ngumu. Ni vigumu kuwa karibu na wale wenye shinda wanapo tuhitaji sisi. Ni vigumu kuwa waminifu mpaka mwisho bila kuwa na aibu tunapo kutana na vishawishi vya hofu. Yesu anatupa nguvu na msaada wa upendo kamili yeye akiwa kama Mchungaji wetu mwema, lakini pia anatuhitaji nasi turudishe upendo huu huu kwake, kwa kuwapatia wengine upendo huu huu mkamilifu. Pale ulipo shindwa na kupungukiwa tunamuomba yeye akuchunge kama mchungaji ili nawe uweze kuwachunga wengine. Mkimbilie mchungaji mwema na amini upendo wake kwako.

Leo, Kanisa zima linatukumbusha hitaji letu la kuomba, kama Yesu mwenyewe alivyo waambia wanafunzi wake, hivyo kwamba "mwombeni Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi katika mavuno yake" (Lk 10: 2). Tangu hapo awali Kanisa “ kwa asili yake ni umisionari" (Ad Gentes, 2), wito wa Ukristo unazaliwa ndani ya watu kutokana na kazi ya umisionari. Kusikia na kufuata sauti ya Kristo Mchungaji mwema, maana yake ni kuruhusi tuvutwe naye na tuongozwe naye, kujiweka wakfu kwake maana yake kumruhusu Roho Mtakatifu kututumia sisi katika mabadiliko haya ya umisionari, na kuamsha ndani yetu tamaa, furaha na ujasiri wa kutoa maisha yetu wenyewe katika utumishi wa Ufalme wa Mungu.

Katika mzizi wa kila wito wa Kikristo tunaona harakati hii ya msingi, ya kuacha nyuma faraja yetu na mambo yote yanayo tupendezesha nafsi zetu na kujikita katika maisha ya Yesu Kristo. Ina maana ya kuondoka, kama Abrahamu, na kuacha sehemu yetu ya asili na kwenda mbele kwa uaminifu, tukijua kwamba Mungu atatuonesha njia ya nchi mpya. Hii "kwenda mbele" isi tazamwe kama ishara ya mpango tu wa maisha ya mtu binafsi, hisia ya mtu, utu wa mtu mwenyewe. Kinyume chake, wale ambao wanamfuata Kristo wanapata uzima kwa wingi kwa kujiweka wenyewe bila kujibakiza katika utumishi wa Mungu na ufalme wake. Wito wa Kikristo kwanza kabisa ni wito wa upendo, upendo ambao hutuvuta sisi na kutuelekeza nje ya sisi wenyewe. Kuitika wito wa Mungu, maana yake kumruhusu yeye atusaidie kujiacha wenyewe kwakuondokana na usalama wetu wa uongo, na kutoka nje na kuenenda kwenye njia inayo ongoza kwa Yesu Kristo, aliye asili na hatima ya maisha yetu na furaha yetu.

Katika siku hizi kwanza tunaombwa tuombee Kanisa liweze kupata wachungaji wema na waadilifu wa kufanya kazi ya Kristo ya kueneza Injili, na kwamba Kanisa liweze kupata vijana wengi wanoitwa kwenye wito wa upadre na utawa ikiwa ni pamoja na watoto wetu wenyewe.

SALA: Baba wa huruma, uliyemtoa mwanao kwa ajili ya wokovu wetu na ambaye anatutia nguvu kila wakati kwa zawadi ya Roho wako, tujaliye sisi jumuiya ya Wakristo tulio hai, upendo na furaha, vilivyo vya muhimu kwa maisha ya kindugu, na vinavyojenga ndani ya wadogo mwamko wa wito wakujitoa wenyewe wakfu kwako na kwa ajili ya wito wa uenezaji wa neno lako. Dumisha ndani ya jumuiya hizi majitoleo ya kutoa katekesi ya kuitika wito huu wakujitoa wakfu kwako. Wajaliye hekima inayohitajika katika maamuzi ya kufuata wito wako, ili katika yote ukuu wa huruma yako ya upendo iweze kungara. Tunaomba Maria, Mama na uliyekuwa kiongozi wa Yesu, utombee. Yesu tunakutumainia wewe. Amina.

Copyright ©2013-2024 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, JUMAPILI, APRILI 21, 2024


MASOMO YA MISA, JUMAPILI, APRILI 21, 2024
DOMINIKA YA 4 YA PASAKA, MWAKA B

SOMO  1
 Mdo.4:8-12

Ndipo Petro, akijaa Roho Mtakatifu, akawaambia, Enyi wakubwa wa watu na wazee wa Israeli, kama tukiulizwa leo habari ya jambo jema alilofanyiwa yule mtu dhaifu, jinsi alivyoponywa, jueni ninyi nyote na watu wote wa Israeli ya kuwa kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye ninyi mlimsulibisha, na Mungu akamfufua katika wafu, kwa jina hilo mtu huyu anasimama ali mzima mbele yenu. Yeye ndiye jiwe lile lililodharauliwa na ninyi waashi, nalo limewekwa kuwa jiwe kuu la pembeni. Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.

Neno la Bwana......................................Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab 118:1,8-9,21-23,26,28-29

(K)Jiwe walilolikataa waashi, Limekuwa jiwe kuu la pembeni

Aleluya. 
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, 
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Ni heri kumkimbilia Bwana 
Kuliko kuwatumainia wanadamu.
Ni heri kumkimbilia BWANA. 
Kuliko kuwatumainia wakuu.

Nitakushukuru kwa maana umenijibu,
Nawe umekuwa wokovu wangu.
Jiwe walilolikataa waashi 
Limekuwa jiwe kuu la pembeni.
Neno hili limetoka kwa Bwana, 
Nalo ni ajabu machoni petu.

Na abarikiwe yeye ajaye kwa jina la Bwana; 
Tumewabarikia toka nyumbani mwa Bwana
Ndiwe Mungu wangu, nami nitakushukuru, 
Ndiwe Mungu wangu, nami nitakutukuza.
Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema, 
Kwa maana fadhili zake ni za milele.


SOMO  2
1Yoh.3:1-2

Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye. Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona kama alivyo.

Neno la Bwana........................................Tumshukuru Mungu. 


Shangilio
Yn 10:14

Aleluya aleluya
Mimi ndimi mchungaji mwema;
nao walio wangu nawajua;
Nao walio wangu wanijua mimi . 
Aleluya


Injili
Yn.10:11-18

Siku ile,Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo. Mtu wa mshahara, wala si mchungaji, ambaye kondoo si mali yake, humwona mbwa-mwitu anakuja, akawaacha kondoo na kukimbia; na mbwa-mwitu huwakamata na kuwatawanya. Yule hukimbia kwa kuwa ni mtu wa mshahara; wala mambo ya kondoo si kitu kwake. kama vile Baba anijuavyo, nami nimjuavyo Baba. Nami nautoa uhai wangu kwa ajili ya kondoo. Ndiposa Baba anipenda, kwa sababu nautoa uhai wangu ili niutwae tena. Hakuna mtu aniondoleaye, bali mimi nautoa mwenyewe. Nami ninao uweza wa kuutoa, ninao na uweza wa kuutwaa tena. Agizo hilo nalilipokea kwa Baba yangu.

Neno la Bwana...........Sifa kwao Ee Kristo. 


Copyright © 2024, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

20th APRIL 2024



 

UNA MANENO YA UZIMA WA MILELE!



“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumamosi, Aprili 20, 2024
Juma la 3 la Pasaka

Mdo 9: 31-42;
Zab 116: 12-17;
Yn 6: 60-69.


UNA MANENO YA UZIMA WA MILELE!


Yohane anataka kutuonesha kwamba Yesu ndiye anayetulisha chakula cha uzima wa Kimungu, kwakutupa sisi maisha yake mwenyewe na mwili wake. Kula mkate na samaki aliowapa Yesu ilikuwa rahisi lakini kusikiliza maneno yake ilikuwa vigumu, baada ya haya Injili inasema wazi kwamba wafuasi wengi walimwacha na wengine waliacha kuambatana naye. Lakini wakati Yesu alipowauliza wale kumi na wawili, kama na wao wanataka kuondoka pia, Petro alijibu, “Bwana tuende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele” Ndio, Petro anatambua japo kuwa si kwahakika sana kipindi hicho, kwamba “Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu”

Swali hili la Yesu kwa Mitume wake ni muhimu sana. Kwa kuwauliza wao moja kwa moja, Yesu anawapa uhuru kamili wa kuchagua. Hawashinikizi kukubali au kuamini alichokuwa amefundisha mara. Hili lilikuwa muhimu kwa sababu kwa kiasi ambacho Yesu anatoa cha kuachia yote ni mwaliko wa kuwa na uhuru kamili, kwa upande wa mitume, kwa mafundisho yake ya utukufu juu ya Ekaristi. Wapo huru kabisa kukubali au kukataa. Ni uhuru huu utawafanya wazame katika Imani yao juu ya Yesu.

Tutafakari leo, juu ya kujikabidhi kwetu kwa Yesu. Tupo huru kabisa kumfuata yeye au kumkataa. Yesu hapendi tumchague na kumfuata nusu nusu. Maneno ya Yesu yana nguvu, yana changamoto na yanahitaji sadaka. Anataka tumwamini yeye na kumfuata kwa moyo wote na kujikabidhi kweli. Ni Yesu mwenyewe mwenye maneno ya uzima wa milele na tunapaswa tukubali maneno yake na kuamini kwa nguvu zetu zote.

Ni neno la Mungu kweli linalo tutakasa na kutuburudisha. Linatupa uzima; kwahiyo kinachotupa uzima ni Neno la Mungu, kwani maneno anayosema Yesu ni roho tena ni uzima. Jumuiya ya Wakristo kama tunavyosikia katika Somo la kwanza leo, walijenga msingi wao juu ya uzima huu walioupokea kutoka kwa Yesu na faraja ya Roho Mtakatifu. Sisi tuna uhai na uzima, ila uzima wetu na maisha yetu tuyaweke ndani ya Bwana wa uzima Yesu Kristo mwenyewe. Ni maneno haya yenye uzima ya Yesu yalioweza kumrudishia uzima Dorcasi kama tunavyosikia katika somo la kwanza.

Sala: Bwana Yesu, ni wewe pekee ninaye kuchagua kukuamini na kukufuata. Nisaidie nikumbatie yote uliyo fundisha na nisaidie kukuchagua kwa uhuru katika maisha yangu ya kila siku. Yesu nakuamini wewe. Amina


Copyright ©2013-2024 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

MASOMO YA MISA, APRILI 20, 2024



MASOMO YA MISA, APRILI 20, 2024
JUMAMOSI, JUMA LA 3 LA PASAKA


SOMO 1
Mdo. 9:31-42

Kanisa lilipata raha katika Uyahudi wote na Galilaya na Samaria, likajengwa, likiendelea na kuongoezeka katika kicho cha Bwana, na faraja ya Roho Mtakatifu.

Hata Petro alipokuwa akizunguka-zunguka pande zote akawatelemkia na watakatifu waliokaa Lida. Akamwona mtu mmoja huko, jina lake Ainea, mtu huyo amelala kitandani miaka minane; maana alikuwa amepooza. Petro akamwambia. Ainea, Yesu Kriso akuponya; ondoka, ujitandikie. Mara akaondoka. Na watu waliokaa Lida na Sharani wakamwona, wakamgeukia Bwana.

Na mwanafunzi mmoja alikuwako Yafa, jina lake Tabitha, tafsiri yake ni Dorkasi (yaani paa); mwanamke huyu alikuwa amejaa matendo mema na sadaka alizozitoa. Ikawa siku zile akaugua, akafa; hata walipokwisha kumwosha, wakamweka orofani. Na kwa kuwa mji wa Lida ulikuwa karibu na Yafa, nao wanafunzi wamesikia ya kwamba Petro yuko huko, wakatuma watu wawili kwake, kumsihi na kusema, Usikawie kuja kwetu.

Petro akaondoka akafuatana nao. Alipofika, wakampeleka juu orofani wajane wote wakasimama karibu naye, wakilia na kumwonyesha zile kanzu na nguo alizozishona Dorkasi wakati ule alipokuwa pamoja nao. Petro akawatoa nje wote, akapiga maogi, akaomba, kisha akaelekea yule maiti, akanena, Tabitha, ondoka. Naye akafumbua macho yake, na alipomwona Petro akajiinua, akaketi. Akampa mkono, akamwinua, hata akiisha kuwaita wale watakatifu na wajane akamweka mbele yao, hali yu hai. Ikajulikana katika mji mzima wa Yafa; watu wengi wakamwamini Bwana.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 116:12-17 (K) 12

(K) Nimrudishie Bwana nini kwa ukarimu wake wote alionitendea?

Nimrudishie Bwana nini
Kwa ukarimu wake wote alionitendea?
Nitakipokea kikombe cha wokovu;
Na kulitangaza jina la Bwana. (K)

Nitaziondoa nadhiri zangu kwa Bwana,
Naam, mbele ya watu wake wote.
Ina thamani machoni pa Bwana
Mauti ya wacha Mungu wake. (K)

Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako,
Mtumishi wako, mwana na mjakazi wako,
Umenifungua vifungo vyangu.
Nitakutolea dhabihu ya kushukuru;
Na kulitangaza jina la Bwana. (K)



SHANGILIO
Kol. 3:1

Aleluya, aleluya,
Mkiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu, Kristo aliko, ameketi mkono wa kuume wa Mungu.
Aleluya.



INJILI
Yn. 6:60:69

Siku ile, watu wengi miongoni mwa wanafunzi wake waliposikia maneno ya Yesu juu ya mkate wa uzima, walisema: Neno hili ni gumu, ni nani awezaye kulisikia? Naye Yesu akafahamu nafsini mwake ya kuwa wanafunzi wake wanalinung’unukia neno hilo, akawaambia, Je! Neno hili linawakwaza? Itakuwaje basi, mmwonapo Mwana wa Adamu akipaa huko alikokuwako kwanza? Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu; maneno hayo niliyowaambia ni roho, tena ni uzima.

Lakini kuna wengine miongoni mwenu wasiomini. Kwa maana Yesu alijua tangu mwanzo ni nani wasioamini, naye ni nani atakayemsaliti. Akasema, kwa sababu hiyo nimewaambia ya kwamba hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu. Kwa ajili ya hayo wengi miongoni mwa wanafunzi wake wakarejea nyuma wasiandamane naye tena.

Basi Yesu akawambia wale Thenashara, Je! Ninyi nanyi mwataka kuondoka? Basi Simoni Petro akamjibu, Bwana! Twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele. Nasi tumesadiki, tena tumejua, ya kuwa wewe ndiwe Mtakatifu wa Mungu.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright © 1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

19th APRIL 2024

 




MAISHA YETU YANATOKA KWA KRISTO!

 


“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Ijumaa, Aprili 19, 2024
Juma la 3 la Pasaka

Mdo 9:1-20;
Zab 117:1-2 (K. Mk 16:15);
Yn  6:52-59.


MAISHA YETU YANATOKA KWA KRISTO!


Mt. Paulo ambaye tunamsikia katika somo la kwanza la leo alikuwa mtu mwenye Elimu ya juu/ busara aliyesoma chini ya mwalimu mkuu Gamaliel. Uongofu wake wa ghafla ulitokea  barabarani akielekea Dameski. Paulo ambaye alikuwa na mambo mengi, lakini akikosa jambo muhimu zaidi ambalo alilipata kupitia ndani ya tukio hili la wongofu. Alimpata Yesu Kristo. Baada ya uzoefu huo Paulo anatangaza, "Kwangu mimi, kuishi ni Kristo"; kama nilivyo, maisha ni Yesu Kristo" au "Naweza kufanya  yote katika Yeye anitiaye nguvu." "Naishi sasa si kwa maisha yangu mwenyewe bali kwa maisha ya Kristo anayeishi ndani yangu."

Mara baada ya Paulo kukutana na Yesu, maisha yake hayakubaki kamwe jinsi yalivyo kuwa mwanzo. Alibadilika kabisa. Alikuwa kiumbe kipya katika Kristo. Nasi pia tunampokea Kristo katika Ekaristi Takatifu. Ni kwa kiasi gani Ekaristi inabadilisha maisha yetu? Ni kwa kiasi gani najitoa mwenyewe kwa Kristo pale anapojitoa mwenyewe kwangu?

Katika somo la Injili, Yesu anasema “msipo ula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake hamna uzima ndani yenu”. Wengi wao walichukizwa na kuanza kuuliza uliza juu ya maneno yake. Inavutia kwamba wakati Yesu anapokutana na maneno makali ya wengine, anajibu tena kwa ujasiri mkubwa zaidi na uwazi zaidi. Hili linamuonesha kuwa mtu wa ujasiri mkubwa, mwenye nguvu na kuelewa. Unafunua pia kwetu sisi ujasiri ambao sisi tunapaswa kuwa nao katika ulimwengu huu. Ulimwengu tunaoishi ni ulimwengu unao kataa ukweli. Unakataa ukweli wa maadili, lakini pia unapinga ukweli wa ndani wa kiroho pia. Ukweli huu wa ndani ni kama uwepo wa uzuri wa Ekaristi Takatifu, umuhimu wa sala za kila siku, unyenyekevu, na kumtegemea Mungu, kuweka mapenzi ya Mungu mbele kuliko kitu chochote nk. Tunapaswa kutambua kuwa kila mara tunapo sogea karibu zaidi na Mungu, ndivyo tunavyozidi kujikabidhi kwake zaidi, na tutakapo hubiri ukweli wa Mungu ndivyo tunavyo upa ulimwengu shinikizo uache kutuiba kutoka kwa Mungu.

Sasa tufanye nini? Tunajifunza kutoka katika ujasiri na nguvu ya Yesu. Tunapojikuta sisi wenyewe tukiwa katika changamoto au tunapo hisi kana kwamba Imani yetu inashambuliwa, ndivyo tunavyo takiwa tuzame ndani zaidi na kuwa waaminifu zaidi na zaidi. Hili litatufanya tuwe na nguvu zaidi na kufanya vishawishi vinayokuja kuwa nafasi ya neema! Chagua kuiga ujasiri na ushupavu wa Bwana wetu na utakuwa chombo chenye kuonekana cha neema na huruma.

Sala: Bwana, ninaomba unipe ujasiri wa nguvu zako . Ninaomba unipe mwangaza katika utume wangu na unisaidie kukutumikia kiaminifu katika kila kitu. Ninaomba nisiwe muoga ninapo kutana na changamoto za maisha bali nitazame hamu yangu ya kukutumikia kwa moyo wangu wote. Yesu nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2024 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

MASOMO YA MISA, APRILI 19, 2024



MASOMO YA MISA, APRILI 19, 2024
IJUMAA, JUMA LA 3 LA PASAKA


SOMO 1
Mdo. 9:1-20

Siku zile, Sauli, akizidi kutisha na kuwaza kuwaua wanafunzi wa Bwana, akamwendea Kuhani Mkuu, akataka ampe barua za kwenda Dameski zilizoandikwa kwa masinagogi, ili akiona watu wa Njia hii, waume kwa wake, awafunge na kuwaleta Yerusalemu.

Hapo alipokuwa akisafiri, ikawa anakaribia Dameski; ghafula ikamwangaza kote kote nuru kutoka mbinguni. Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, Sauli, Sauli, mbona waniudhi? Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema, Mimi ndimi Yesu unayeniudhi wewe. Lakini simama, uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda. Na wale watu waliosafiri pamoja naye wakasimama kimya, wakiisikia sauti, wasione mtu. Sauli akainuka katika nchi, na macho yake yalipofumbuka, hakuona kitu; wakamshika mkono wakamleta mpaka Dameski. Akawa siku tatu haoni; hali, wala hanywi.

Basi palipokuwapo Dameski mwanafunzi jina lake Anania. Bwana akamwambia katika maono, Anania. Akasema, Mimi hapa, Bwana. Bwana akamwambia, Simama, enenda zako katika njia iitwayo Nyofu, ukaulize katika nyumba ya Yuda mtu aitwaye Sauli, wa Tarso; maana, angalia, anaomba; naye amemwona mtu, jina lake Anania, akiingia, na kumwekea mikono juu yake, apate kuona tena.

Lakini Anania akajibu, Bwana, nimesikia habari za mtu huyu kwa watu wengi, mabaya mengi aliyowatenda watakatifu wako Yerusalemu; hata hapa ana amri itokayo kwa wakuu wa makuhani awafunge wote wakuitiao Jina lako. Lakini Bwana akamwambia, Nenda tu; kwa maan ahuyu ni chombo kiteule kwangu, alichukue Jina langu mbele ya Mataifa, na wafalme, na wana wa Israeli. Maana nitamwonyesha yalivyo mengi yatakayompasa kuteswa kwa ajili ya Jina langu. Anania akaenda zake, akaingia mle nyumbani, akamwekea mikono akisema, Ndugu, Sauli, Bwana amenituma, Yesu yeye aliyekutokea katika njia uliyoijia, upate kuona tena, ukajazwe Roho Mtakatifu. Mara vikaanguka machoni pake vitu kama magamba, akapata kuona, akasimama, akabatizwa, akala chakula, na kupata nguvu.

Akawa huko siku kadha wa kadha pamoja na wanafunzi walioko Dameski. Mara akamhubiri Yesu katika masinagogi, kwamba yeye ni Mwana wa Mungu.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 117 (K) Mk. 16:15

(K) Enendeni ulimwenguni mwote,
mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.

Enyi mataifa yote, msifuni Bwana,
Enyi watu wote, mhimidini. (K)

Maana fadhili zake kwetu sisi ni kuu,
Na uaminifu wa Bwana ni wa milele. (K)



SHANGILIO
Rum. 6:9

Aleluya, aleluya,
Kristo akiisha kufufuka katika wafu hafi tena, wala mauti haimtawali tena. Aleluya.



INJILI
Yn. 6:52-59

Siku ile, Wayahudi walishindana wao kwa wao wakisema, Awezaje mtu huyu kutupa sisi mwili wake ili tuule?

Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu. Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho. Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli. Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake. Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, nami ni hai kwa Baba; kadhalika naye mwenye kunila atakuwa hai kwa mimi. Hiki ndicho chakula kishukacho kutoka mbinguni; si kama mababa walivyokula, wakafa; bali akilaye chakula hicho ataishi milele.

Maneno hayo aliyasema katika sinagogi, alipokuwa akifundisha, huko Kapernaumu.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.


Copyright © 2024, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

18th APRIL 2024




 

KUVUTWA KWA YESU!


“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Alhamisi, Aprili 18, 2024
Juma la 3 la Mwaka

Mdo 8:26-40;
Zab 66:8-9,16-17,20 (K. 1);
Yn 6:44-51.


KUVUTWA KWA YESU!

Karl Rahner anasema, “kila ninapo ongea kuhusu mimi najikuta nikiongelea kuhusu Mungu, na kila ninapo ongelea kuhusu Mungu najikuta naongea kuhusu mimi”. Safari ya maisha yetu pia karibia ni kuvuta kila kitu na kila mtu kwangu. Katika ulimwengu huu ambao kila mtu yupo na shughuli zake ni rahisi sana kuruhusu sauti mbali mbali zituharibu. Ni rahisi kusikia kusukumwa huku na kule katika ulimwengu na mambo yake yote. Ulimwengu umekuwa mzuri sana ukiteka mipango yetu yote na kutupatia kuridhika kwa haraka lakini utatuacha bila kitu.

Lakini sauti ya Mungu na mwaliko wake ni tofauti. Unapatikana katika ukimya wa ndani. Lakini haina maana kwamba unapaswa kuwa katika monasteri ili kupata ukimya huu wa ndani. Unapatika katika uaminifu mkubwa katika sala kila siku, na tabia ya kurudi kwa Mungu kila wakati katika vitu vyote. Unapatikana tunapo jibu wito wa Mungu, na kuifuata, na kurudia tena kila mara. Hili linajenga tabia ya kuvutwa karibu, kusikia, na kuitika na kuvutwa karibu na kusikiliza na kuitika tena na tena.

Katika Injili ya leo, tunatambua kuwa tumeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu, na tunavutwa daima kwa Mungu. Ndani kabisa mwa moyo wa Mwanadamu, ana mtamani Mungu. Ndio maana Yesu anasema wazi kwamba “hakuna ajaye kwangu asipovutwa na Baba yangu” (Yn 6: 44). Katika somo la kwanza tunamuona Ofisa wa Ethiopia wakati akisoma chuo cha nabii Isaya, anakutana na ukweli katika Maandiko Matakatifu kwa msaada wa Filipo, na baadae anamkubali Yesu kama Mkombozi na Bwana.

Tutenge muda tuvutwe kwa Yesu. Tenga muda mchache au zaidi kila siku wa ukimya. Funga macho na jisikilize. Msikilize Mungu akiongea na wewe. Wakati akikuvuta kwake itika kwa ukarimu. Huu ndio uchaguzi mzuri kabisa ambao waweza kufanya kila siku!

Sala: Bwana, naomba univute karibu ili niweze kutambua sauti yako. Ninapo kusikia ukiita, nisaidie niweze kukuitikia kwa ukarimu. Maisha yangu ni yako, Bwana mpendwa. Yesu, nakuamini wewe. Amina.


Copyright ©2013-2024 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com