Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu
JE, UNAKUWA NA WIVU MWENZAKO ANAPO FANIKIWA?
“ASALI
ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari
ya kila siku
Jumatano,
Agosti 20, 2025
Juma
la 20 la Mwaka
___________________
Amu
9: 6-15;
Zab
20: 2-7;
Mt
20:1-16
___________________
JE,
UNAKUWA NA WIVU MWENZAKO ANAPO FANIKIWA?
Somo
la Injili ni maelezo ya mfano wa wakulima katika shamba la mizabibu. Mfano
unaeleza ni kwa jinsi ghani mwenye shamba alivyoenda sokoni kwa muda tofauti
tofauti na kutafuta wafanyakazi hata wakati wa saa kumi na moja jioni. Wakati
wale wafanyakazi wa kwanza walikuwa wamekubaliana kabisa kwamba watapewa
mshahara wa dinari moja, na wakati wengine wakiambiwa watapewa kilicho haki
yao. Wakati wa malipo macho yalikuwa kwa wale ambao wameajiriwa wa mwisho,
wakati wale wa kwanza wakilipwa mbele ya wengine wote. Wa mwisho wanalipwa sawa
kama walivyokubaliana na mwenye shamba. Ingawaje mfano hausemi ni kiasi gfhani
cha kazi kilicho fanyika au pengine wale wa mwisho walifanya kazi haraka haraka
kiasi cha kuwafikia wale wa kwanza? Hausemi. Hali hii inaleta changamoto!
Lakini Yesu alitaka kusema kwamba wadhambi na watoza ushuru walio tubu watakuwa
pia katika hali moja na wale ambao wameshika sheria tangu mwanzoni. Mfano huu
unataka kutufundisha kitu kwamba, Mungu haangalii ni kwa muda ghani uliofanya
kazi, bali ni kwa jinsi ghani ulivyo mwaminifu katika kazi.
Kwanza
kabisa, hali hii inashawishi kila mtu kuwa na wivu. Wivu ni aina ya kuwa na
huzuni au kutokufurahi kwasababu ya mtu mwingine kufanikiwa. Pengine tunaweza
kuelewa wivu waliokuwa nao wale waliofanya kazi siku nzima. Ukweli si kwamba ni
kitu ghani walichopokea bali ni wale wengine wamepokea kiasi hicho hicho kama
wao, hivyo inaonekana kuwa kama sio haki. Tofatuti ni kwamba wale wa kwanza
wamepokea kile walicho kifanyia kazi siku nzima, na wengine wamepokea sawa na
hao wengine kwasababu ya ukaribu wa Bwana shamba.
Kama
sisi tutajiweka na lile kundi linalo lalamika, ni vizuri tuangalie misukumo
yetu. Je, sisi tunaweza kujazwa furaha na Amani kwasababu ya ndugu zetu kufanikiwa?
Je, waweza kumshukuru Mungu na kumwambia asante wakati ndugu au mwingine alivyo
fanikiwa? Wivu mbaya ni dhambi, na ni dhambi ambayo inatuacha tukiwa hatuja
ridhika na wenye huzuni. Njia pekee ambayo tunaweza kushinda ni kufurahia
mafanikio ya ndugu zetu.
Sala:
Bwana, ninatenda dhambi na ninakubali kwamba nina wivu moyoni mwangu.
Ninakushukuru wewe kwa kunisaidia kuliona hili ninakuomba unisaidie sasa
nikabidhi kwako. Tafadhali nisaidie kuondoa kwa kuwa na shukrani kwa neema na
huruma yako unawajalia wengine. Yesu, nakuamini wewe. Amina
MASOMO YA MISA, JUMATANO, AGOSTI 20, 2025
MASOMO
YA MISA,
JUMATANO,
AGOSTI 20, 2025
JUMA
LA 20 LA MWAKA
Kumbukumbu
ya Mtakatifu Bernardo
________
SOMO
I
Amu
9: 6-15
Watu
wote wa Shekemu walikusanyika pamoja, na jamaa yote ya Milo, wakaenda na
kumtawaza Abimeleki awe mfalme, karibu na huo mgandi ulio karibu na ngome iliyo
katika Shekemu.
Kisha
walipomwambia huyo Yothamu, yeye akaenda, akasimama juu ya kilele cha kilima
cha Gerizimu, akapaza sauti yake, akapiga kelele, na kuwaambia:
Nisikieni
mimi, enyi watu wa Shekemu, ili kwamba Mungu naye apate kuwasikia ninyi.
Siku
moja miti ilitoka ili kuutia mmoja mafuta uwe mfalme juu yao; ikauambia mti
mzeituni, Tawala wewe juu yetu.
Lakini
huo mzeituni ukaiambia, Je! Niache mafuta yangu, ambayo kwangu mimi watu
wamheshimu Mungu na wanadamu, ili niende nikayongeyonge juu ya miti?
Kisha
miti ikauambia mtini, Njoo wewe, utawale juu yetu.
Lakini
huo mtini ukaiambia, Je! Niuache utamu wangu, na matunda yangu mazuri, niende
nitayonge-yonge juu ya miti?
Kisha
miti ikauambia mzabibu, Njoo wewe, utawale juu yetu.
Huo
mzabibu nao ukaiambia, Je! Niiache divai yangu, ambayo humfurahisha Mungu na
wanadamu, ili niende nikayonge-yonge juu ya miti?
Ndipo
hiyo miti yote ikauambia mti wa miiba, Njoo wewe, utawale juu yetu.
Huo
mti wa miiba ukaiambia miti, Kwamba ninyi mwanitia mafuta niwe mfalme juu yenu
kwelikweli, basi njoni mtumaini kivuli changu; na kwamba sivyo, na utoke moto
katika mti wa miiba na kuitekete mierezi ya Lebanoni.
Neno
la Bwana...Tumshukuru Mungu
________
WIMBO
WA KATIKATI
Zab.
21: 1-6
(K)
Ee Bwana, mfalme atazifurahia nguvu zako.
Ee
Bwana, mfalme atazifurahia nguvu zako,
Na
wokovu wako ataufanyia shangwe nyingi sana.
Umempa
haja ya moyo wake,
Wala
hukumzuilia matakwa ya midomo yake. (K)
Maana
umesogezea Baraka za heri,
Umemvika
taji ya dhahabu safi kichwani pake.
Alikuomba
uhai, ukampa.
Muda
mrefu wa siku nyingi, milele na milele. (K)
Utukufu
umemsogezea Baraka za heri,
Umemvika
taji ya dhahabu safi kichwani pake.
Alikuomba
uhai, ukampa.
Muda
mrefu wa siku nyingi, milele na milele. (K)
________
SHANGILIO
Zab
119:18
Aleluya,
aleluya,
Unifumbue
macho yangu niyatazame
maajabu
yatokayo katika sheria yako.
Aleluya.
________
INJILI
Mt.
20: 1-16
Yesu
aliwaambia wafuasi wake: Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu mwenye nyumba,
aliyetoka alfajiri kwenda kuajiri wakulima awapeleke katika shamba lake la
mizabibu. Naye alipokwisha kupatana na wakulima kuwapa kutwa dinari,
aliwapeleka katika shamba lake la mizabibu. Akatoka mnamo saa tatu, akaona
wengine wamesimama sokoni wasiokuwa na kazi; na hao nao akawaambia, Enendeni
nanyi katika shamba langu la mizabibu, na iliyo haki nitawapa. Wakaenda.
Akatoka
tena mnamo saa sita na saa kenda, akafanya vile vile. Hata kama saa kumi na
moja akatoka, akauta wengine wamesimama, akawaambia, Mbona mmesimama hapa
mchana kutwa bila kazi? Wakamwambia, Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri.
Akawaambia enendeni nanyi katika shamba la mizabibu.
Kulipokuchwa,
yule bwana wa shamba akamwambia masimamizi wake, Waite wakulima, uwalipe ujira
wao, ukianzia wa mwisho hata wa kwanza. Na walipokuja wale wa saa kumi na moja,
walipokea kila mtu dinari. Na wale wa kwanza walipokuja, walidhani kwamba
watapokea zaidi; na hao pia wakapokea kila mtu dinari.
Basi
wakiisha kuipokea, wakamnung’unukia mwenye nyuma, wakisema, Hao wa mwisho
wametenda kazi saa moja tu, nawe umewasawazisha na sisi tuliostahimili taabu na
hari za mchana kutwa. Naye akamjibu mmoja wao, akamwambia, Rafiki, sikudhulumu;
hukupatana nami kwa dinari? Chukua iliyo yako, uende zako; napenda kumpa huyu
wa mwisho sawa na wewe. Si halali yangu kutumia vilivyo vyangu kama nipendavyo?
Au jicho lako limekuwa ovu kwa sababu ya mimi kuwa mwema Vivyo hivyo wa mwisho
watakuwa wa kwanza, na wa kwanza watakuwa wa mwisho.
Neno
la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo
Copyright
© 2025, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora
– Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com
KUACHA YOTE NA KUMFUATA KRISTO!
ASALI
ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari
ya kila siku
Jumanne,
Agosti 19, 2025
Juma
la 20 la Mwaka wa Kanisa
Amu:
6:11-24
Zab:
85:8-13
Mt
19:23- 30
KUACHA
YOTE NA KUMFUATA KRISTO!
Kilele
cha mwisho kabisa cha mwanadamu ni kujua, kupenda, kumtumikia Mungu na
kufurahia maisha ya milele pamoja naye daima. Na Mungu anapenda kutushirikisha
uzima huu wa milele. Ni zawadi kutoka kwa Mungu. Hatuwezi kupata uzima huu kwa
nguvu za kibinadamu. Tungeachiwa sisi tu, ingekuwa vigumu sana kwetu sisi
kuupata. Lakini kwa neema ya Mungu yote yanawezekana. Lakini, mali na utajiri
vinaonekana viashiria vinavyo hatarisha kutokuupata ufalme huu wa milele.
Katika ulimwengu huu wa sasa wenye mambo mengi inakuwa vigumu kwa wengine
kukwepa hili. Ni jambo kubwa la kweli “kuacha yote” lakini kubwa zaidi
“kumfuata Yesu”.
Kumfuata
Yesu ni kazi yetu. Katika hili linabeba ukombozi wa mwanadamu, lakini hatuwezi
kumfuata Kristo kama hatutaacha yote yanayotufunga tushindwe kumfuata. Nabii
Ezekiel katika somo la kwanza anatoa angalisho kwa mji wa Tiro na viongozi wake
waliopata mafanikio makubwa na nguvu. Wameweka ulinzi wao na Imani yao katika
utajiri na mali ambavyo vimegeuka kuwa miungu yao.
Lakini
Petro anasema, “tumeacha yote” sio tuu vitu vya ulimwengu, lakini pia tamaa
zinazopendwa na mioyo yetu. Wanaobaki wakiwa wameshikilia baadhi ya vitu
inakuwa hawajaacha yote. Kwanini anatoa ujumbe mkali namna hiyo kwa matajiri?
Kwanini Yesu anaongea sana kuhusu mali? Ni kwasababu mali inaweza kutufanya
tusiwe huru au kutupa uhuru wa ouongo. Wengine wameshindwa kumfuata Yesu
kwasababu ina maana ya kuacha baadhi ya uhusiano, na wengine kama yule tajiri,
ni kwasababu watapoteza nafasi yao ya heshima au njia zao za kupata mali. Wewe
je?
Sala:
Bwana, naomba nikufanye wewe wa kwanza katika maisha yangu na nikuchague wewe
kwa uhuru kamili hata kama kukufuata inagarimu.
Copyright
©2013-2025 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com
MASOMO YA MISA, JUMANNE, AGOSTI 19, 2025
MASOMO YA MISA, JUMANNE, AGOSTI 19, 2025
JUMA LA 20 LA MWAKA
JUMA LA 20 LA MWAKA
________
SOMO I
Amu 6: 11-24
Malaika wa Bwana alienda akaketi chini ya mwaloni uliokuwa katika Ofra, uliokuwa mali yake Yoashi, Mwabiezeri;na mwanawe Gideoni alikuwa akipepeta ngano ndani ya shinikizo, ili kuficha machoni pa Wamidiani. Malaika wa bwana akamtokea, akamwambia, Bwana yu pamoja nawe,Ee shujaa. Gideoni akamwambia, Ee Bwana wangu,ikiwa bwana yu pamoja nasi na mbona mambo haya yote yametupata? Yako wapi matendo yake ya ajabu, waliotuhafithia babu zetu,wakisema, Je! Siye bwana aliyetuleta huku kutoka Misri? Ila sasa ametutupa,naye ametutia katika mikono ya Midiani. Bwana akamtazama, akasema,enenda kwa uwezo wako huu, ukawaokoe Israeli na mkono wa Midiani. Je! Si mimi ninayekutuma? Akamwambia, Ee Bwana, nitawaokoa Israeli kwa jinsi gani? Tazama, jamaa zangu ndio walio maskini sana katika Manase, na mimi ndimi niliye mdogo katika nyumba ya baba yangu. Bwana akamwambia, hakika nitakuwa nawe, nawe utawapiga Wamiadini kama mtu mmoja. Naye akamwambia, kama nimepata kibali mbele za macho yako, basi unionyeshe ishara, ya kuwa ndiwe wewe unayesema nami. Tafadhali usiondoke hapa hata nikujue, nikatoe zawadi yangu, na kuiweka mbele zako.
Akasema, Nitangoja hata utakaporudi. Basi Gideoni akainhia ndani,akaanda mwna-mbuzi, na mikate isiyotiwa chachu, ya efa ya unga;akaitia ile nyama katika kikapu,akautia mchuzi katika Nyungu, akamletea hapo nje chini ya mwaloni, akampa. Naye Malaika wa Mungu akamwambia, itwae nyama na mikate isiyotiwa chachu uiweke juu ya mwamba huu, ukaumwage huu mchuzi. Akafanya hivyo. Ndipo malaika wa bwana akanyosha ncha ya fimbo ile iliyokuwa mkononi mwake, akaigusa ile nyama na mikate;malaika wa bwana akaondoka mbele ya macho yake. Gideoni akaona ya kuwa ni malaika wa bwana. Gideoni akasema,Ole wangu, Ee Bwana Mungu!kwa kuwa nimemwona Bwana uso kwa uso . Bwana, akamwambia,Amani iwe pamoja nawe;usiogope hutakufa. Ndipo Gideoni akamjengea bwana madhabahu hapo, akaita jina lake, Yehova shalomu; hata hivi leo iko huko Ofra ya Waabiezeri.
Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu
Zab. 85: 8, 10-13
(K) Bwana atawambia watu wake amani.
Fadhili zake na uaminifu vitakutana;
uadilifu na amani vitaungana.
Uaminifu utachipuka katika nchi;
uadilifu utashuka toka mbinguni. (K)
Mwenyezi-Mungu atatuletea fanaka,
na nchi yetu itatoa mazao yake mengi.
Uadilifu utamtangulia Mungu
na kumtayarishia njia yake. (K)
________
SHANGILIO
1 Thes. 2:13
Aleluya, aleluya,
Lipokeeni neno la Mungu,
siyo kama neno la wanadamu,
bali kama neno la Mungu.
Aleluya
________
INJILI
Mt. 19: 23-30
Yesu aliwambia Wanafunzi wake, Amini,nawaambieni, ya kwamba itakuwa shida tajiri kuingia katika ufalme wa mbinguni. Nawambia tena, ni rahisi zaidi kwa Ngamia kupenya tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu. Wanafunzi wasiposikia, walishangaa mno, wakisema, Ni nani basi awezaye kuokoka? Yesu akawakazia macho, akawambia, kwa mwanadamu hilo haliwezekani; bali kwa Mungu yote yawezekana. Ndipo Petro akajibu, akamwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata; tutapata nini basi? Yesu akawambia, Amini, nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya, atakapoketi Mwana wa Adamu katika kiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli. Na kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu wa kiume au wa kike, au baba, au mama, au watoto au mashamba, kwa ajili ya jina langu, atapokea mara mia, na kuurithi uzima wa milele. Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.
Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo
________
SOMO I
Amu 6: 11-24
Malaika wa Bwana alienda akaketi chini ya mwaloni uliokuwa katika Ofra, uliokuwa mali yake Yoashi, Mwabiezeri;na mwanawe Gideoni alikuwa akipepeta ngano ndani ya shinikizo, ili kuficha machoni pa Wamidiani. Malaika wa bwana akamtokea, akamwambia, Bwana yu pamoja nawe,Ee shujaa. Gideoni akamwambia, Ee Bwana wangu,ikiwa bwana yu pamoja nasi na mbona mambo haya yote yametupata? Yako wapi matendo yake ya ajabu, waliotuhafithia babu zetu,wakisema, Je! Siye bwana aliyetuleta huku kutoka Misri? Ila sasa ametutupa,naye ametutia katika mikono ya Midiani. Bwana akamtazama, akasema,enenda kwa uwezo wako huu, ukawaokoe Israeli na mkono wa Midiani. Je! Si mimi ninayekutuma? Akamwambia, Ee Bwana, nitawaokoa Israeli kwa jinsi gani? Tazama, jamaa zangu ndio walio maskini sana katika Manase, na mimi ndimi niliye mdogo katika nyumba ya baba yangu. Bwana akamwambia, hakika nitakuwa nawe, nawe utawapiga Wamiadini kama mtu mmoja. Naye akamwambia, kama nimepata kibali mbele za macho yako, basi unionyeshe ishara, ya kuwa ndiwe wewe unayesema nami. Tafadhali usiondoke hapa hata nikujue, nikatoe zawadi yangu, na kuiweka mbele zako.
Akasema, Nitangoja hata utakaporudi. Basi Gideoni akainhia ndani,akaanda mwna-mbuzi, na mikate isiyotiwa chachu, ya efa ya unga;akaitia ile nyama katika kikapu,akautia mchuzi katika Nyungu, akamletea hapo nje chini ya mwaloni, akampa. Naye Malaika wa Mungu akamwambia, itwae nyama na mikate isiyotiwa chachu uiweke juu ya mwamba huu, ukaumwage huu mchuzi. Akafanya hivyo. Ndipo malaika wa bwana akanyosha ncha ya fimbo ile iliyokuwa mkononi mwake, akaigusa ile nyama na mikate;malaika wa bwana akaondoka mbele ya macho yake. Gideoni akaona ya kuwa ni malaika wa bwana. Gideoni akasema,Ole wangu, Ee Bwana Mungu!kwa kuwa nimemwona Bwana uso kwa uso . Bwana, akamwambia,Amani iwe pamoja nawe;usiogope hutakufa. Ndipo Gideoni akamjengea bwana madhabahu hapo, akaita jina lake, Yehova shalomu; hata hivi leo iko huko Ofra ya Waabiezeri.
Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu
________
WIMBO WA KATIKATI Zab. 85: 8, 10-13
(K) Bwana atawambia watu wake amani.
Fadhili zake na uaminifu vitakutana;
uadilifu na amani vitaungana.
Uaminifu utachipuka katika nchi;
uadilifu utashuka toka mbinguni. (K)
Mwenyezi-Mungu atatuletea fanaka,
na nchi yetu itatoa mazao yake mengi.
Uadilifu utamtangulia Mungu
na kumtayarishia njia yake. (K)
________
SHANGILIO
1 Thes. 2:13
Aleluya, aleluya,
Lipokeeni neno la Mungu,
siyo kama neno la wanadamu,
bali kama neno la Mungu.
Aleluya
________
INJILI
Mt. 19: 23-30
Yesu aliwambia Wanafunzi wake, Amini,nawaambieni, ya kwamba itakuwa shida tajiri kuingia katika ufalme wa mbinguni. Nawambia tena, ni rahisi zaidi kwa Ngamia kupenya tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu. Wanafunzi wasiposikia, walishangaa mno, wakisema, Ni nani basi awezaye kuokoka? Yesu akawakazia macho, akawambia, kwa mwanadamu hilo haliwezekani; bali kwa Mungu yote yawezekana. Ndipo Petro akajibu, akamwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata; tutapata nini basi? Yesu akawambia, Amini, nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya, atakapoketi Mwana wa Adamu katika kiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli. Na kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu wa kiume au wa kike, au baba, au mama, au watoto au mashamba, kwa ajili ya jina langu, atapokea mara mia, na kuurithi uzima wa milele. Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.
Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo
________
Copyright © 2025, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
TUNAITWA KUWA MASKINI WA ROHO
“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya kila siku
Jumatatu, Agosti 18, 2025
Juma la 20 la Mwaka
___________________
Amu 2: 11-19;
Zab 106: 34-37, 39-40, 43-44 (R) 4;
Mt 19: 16-22
___________________
TUNAITWA KUWA MASKINI WA ROHO
Tunaishi katika ulimwengu ambao ni rahisi kuchukuliwa na mali au vitu na hivyo kupoteza mueleke wa kila kitu na na wa wengine. Sisi twaweza kuingia katika kujali mali kuwa ndio mwisho wa kila kitu. “kama unataka kuwa mkamilifu, uza vyote ulivyo navyo na uwape maskini, na utakuwa na hazina mbinguni. Alafu, njoo unifuate”. Wakati kijana huyu mdogo alivyo sikia hivyo alihuzunika sana kwani alikua na mali nyingi.
Yesu anawaita baadhi ya watu katika hali ya kawaida wauze vyote walivyo navyo. Na wote wale wanao tambua wito huu na kujitoa katika kuacha kushikamana na mali, wanapata uhuru mkubwa. Wito wao ni alama ya ndani ya kila mmoja wetu, wito wa ndani ambao kila mmoja wetu amepewa. Lakini kwa wengine je, Bwana anawaitaje? Ni kwa kuwa maskini wa roho. Kwa kuwa “maskni wa roho” ni katika hali hiyo Bwana alikuwa anawaalika kuachilia yote ya malimwengu na kuacha kujifungamanisha nayo, kama hawa waliofanya katika hali ya vitendo. Tofati iliopo ni kwasababu wito wa mmoja ni wa ndani na wa njee, na wengine ni kwa ndani tu. Lakini inapaswa kuwa kamili.
Umaskini wa roho ni kwamba tunatambua Baraka tunazozipata kwa kujinasua kwa kutokushikamana na mali za ulimwengu huu. Mali sio mbaya. Lakini ni rahisi kushikwa na vitu vya ulimwengu. Mara nyingi tunakuwa na vishawishi na kufikiri kwamba kadiri tunavyokuwa na mali nyingi ndivyo tunavyokuwa na raha zaidi. Lakini sio kweli, “aliye na vingi hatosheki”.
Tafakari leo juu ya wito ulioitiwa wa kuishi huku Ulimwenguni bila kujifunganisha na mali. Mali na vitu vingine ni ishara tu ya njee ya kukusaidia kupata uzima wa milele katika malengo ya maisha. Na hili litakuwa na maana kwamba utapata unayo hitaji na kukwepa kuwa na vingi, na hasa kukwepa kujishika na malimwengu kutoka ndani.
Sala: Bwana, ninatamani kuacha yote yanayo nifunga. Ninajitoa kwako kama sadaka ya kiroho. Pokea yote niliyonayo na nisaidie mimi niweze ku tumia katika hali ambayo wewe mwenyewe unatamani. Katika kuachilia huko niweze kuvumbua utajiri wa kweli ulioniwekea mimi. Yesu, nakuamini wewe. Amina
Jumatatu, Agosti 18, 2025
Juma la 20 la Mwaka
___________________
Amu 2: 11-19;
Zab 106: 34-37, 39-40, 43-44 (R) 4;
Mt 19: 16-22
___________________
TUNAITWA KUWA MASKINI WA ROHO
Tunaishi katika ulimwengu ambao ni rahisi kuchukuliwa na mali au vitu na hivyo kupoteza mueleke wa kila kitu na na wa wengine. Sisi twaweza kuingia katika kujali mali kuwa ndio mwisho wa kila kitu. “kama unataka kuwa mkamilifu, uza vyote ulivyo navyo na uwape maskini, na utakuwa na hazina mbinguni. Alafu, njoo unifuate”. Wakati kijana huyu mdogo alivyo sikia hivyo alihuzunika sana kwani alikua na mali nyingi.
Yesu anawaita baadhi ya watu katika hali ya kawaida wauze vyote walivyo navyo. Na wote wale wanao tambua wito huu na kujitoa katika kuacha kushikamana na mali, wanapata uhuru mkubwa. Wito wao ni alama ya ndani ya kila mmoja wetu, wito wa ndani ambao kila mmoja wetu amepewa. Lakini kwa wengine je, Bwana anawaitaje? Ni kwa kuwa maskini wa roho. Kwa kuwa “maskni wa roho” ni katika hali hiyo Bwana alikuwa anawaalika kuachilia yote ya malimwengu na kuacha kujifungamanisha nayo, kama hawa waliofanya katika hali ya vitendo. Tofati iliopo ni kwasababu wito wa mmoja ni wa ndani na wa njee, na wengine ni kwa ndani tu. Lakini inapaswa kuwa kamili.
Umaskini wa roho ni kwamba tunatambua Baraka tunazozipata kwa kujinasua kwa kutokushikamana na mali za ulimwengu huu. Mali sio mbaya. Lakini ni rahisi kushikwa na vitu vya ulimwengu. Mara nyingi tunakuwa na vishawishi na kufikiri kwamba kadiri tunavyokuwa na mali nyingi ndivyo tunavyokuwa na raha zaidi. Lakini sio kweli, “aliye na vingi hatosheki”.
Tafakari leo juu ya wito ulioitiwa wa kuishi huku Ulimwenguni bila kujifunganisha na mali. Mali na vitu vingine ni ishara tu ya njee ya kukusaidia kupata uzima wa milele katika malengo ya maisha. Na hili litakuwa na maana kwamba utapata unayo hitaji na kukwepa kuwa na vingi, na hasa kukwepa kujishika na malimwengu kutoka ndani.
Sala: Bwana, ninatamani kuacha yote yanayo nifunga. Ninajitoa kwako kama sadaka ya kiroho. Pokea yote niliyonayo na nisaidie mimi niweze ku tumia katika hali ambayo wewe mwenyewe unatamani. Katika kuachilia huko niweze kuvumbua utajiri wa kweli ulioniwekea mimi. Yesu, nakuamini wewe. Amina
Copyright ©2013-2025 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
MASOMO YA MISA, JUMATATU, AGOSTI 18, 2025
MASOMO YA MISA, JUMATATU, AGOSTI 18, 2025
JUMA LA 20 LA MWAKA
JUMA LA 20 LA MWAKA
________
SOMO I
Amu 2: 11-19
Wana wa Israeli walifanya yaliyokuwa ni maovu mbele za macho ya Bwana, nao wakawatumikia Mabaali. Wakamwacha Bwana, Mungu wa baba zao, aliyewaleta kutoka katika nchi ya Misri, wakafuata miungu mingine, baadhi ya miungu ya watu wale waliokaa karibu nao pande zote, wakajiinamisha mbele yao; wakamkasirisha Bwana, akaghadhibika. Wakamwacha Bwana, wakamtumikia Baali na Maashtorethi.
Hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye ikawatia katika mikono ya watu waliowateka nyara, akawauza na kuwatia katika mikono ya adui ao pande zote; hata wasiweze tena kusimama mbele ya adui zao. Kila walikokwenda, mkono wa Bwana ulikuwa juu yao kuwatenda mabaya, kama Bwana alivyosema, na kama Bwana alivyowaapia; nao wakafadhaika sana.
Kisha Bwana akawainua waamuzi, waliowaokoa na mikono ya watu hao waliowateka nyara. Lakini nawakuwasikiliza hao waamuzi wao, maana walifanya uasherati kwa kuifuata miungu mingine wakajiinamisha mbele yao; wakageuka upesi, na kuiacha njia ile waliyoiendea baba zao, waliozitii amri za Bwana; bali wao hawakufanya hivyo. Na wakati Bwana alipowainulia waamuzi, ndipo Bwana alikuwa pamoja na mwamuzi huyo, akawaokoa na mikono ya adui zao siku zote za mwamuzi huyo; maana Bwana alighairi kwa ajili ya kuugua kwao kwa sababu ya watu wale waliowaonea na kuwasumbua.
Lakini ikawa, wakati alipokufa mwamuzi huyo, wakarudi nyuma wakafanya maovu kuliko baba zao. kwa kuifuata miungu mingine ili kuitumikia, na kuinama mbele yao; hawakuacha matendo yao, wala njia zao za ukaidi.
Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 106: 34-37, 39-40, 43-44 (K) 4
(K) Ee Bwana, unikumbuke mimi,
kwa kibali uliyo nayo kwa watu wako.
Hawakuwaharibu watu wa nchi
Kama Bwana alivyowaambia;
Bali walijkhanganya na mataifa,
Wakajifunza matendo yao.(K)
Wakazitumikia sanamu zao,
Nazo zikawa mtego kwao.
Naam. walitoa wana wao na binti zao
Kuwa dhabihu kwa mashetani. (K)
Ndivyo walivyotiwa uchafu kwa kazi zao,
Wakafanya uasherati kwa matendo yao.
Hasira ya Bwana ikawaka juu ya watu wake,
Akauchukia urithi wake. (K)
Mara nyingi aliwaponya,
Bali walikuwa wakimwasi kwa mashauri yao,
Wakadhilika katika uovu wao.
Lakini aliyaangalia mateso yao,
Aliposikia kilio chao. (K)
________
SHANGILIO
1 Thes. 2:13
Aleluya, aleluya,
Lipokeeni neno la Mungu,
siyo kama neno la wanadamu,
bali kama neno la Mungu.
Aleluya
________
INJILI
Mt. 19: 16-22
Mtu mmoja alimwendea Yesu akamwambia, Mwalimu, nitende jambo gani jema, ili nipate uzima wa milele? Akamwambia, Kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja. Lakini ukitaka kuingia katika uzima, zishike amri. Akamwambia, Zipi? Yesu akasema, Ni hizi, Usiue, Usizini, Usiibe, Lsishuhudie uongo, Waheshimu baba yako na mama yako, na, Mpende jirani yako kama nafsi yako.
Yule kijana akamwambia, Haya yote nimeyashika; nimepungukiwa na nini tena? Yesu akamwambia, Ukitaka kuwa mkamilifu, enenda ukauze ulivyo navyo, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate. Yule kijana alipolisikia neno lile, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo
________
SOMO I
Amu 2: 11-19
Wana wa Israeli walifanya yaliyokuwa ni maovu mbele za macho ya Bwana, nao wakawatumikia Mabaali. Wakamwacha Bwana, Mungu wa baba zao, aliyewaleta kutoka katika nchi ya Misri, wakafuata miungu mingine, baadhi ya miungu ya watu wale waliokaa karibu nao pande zote, wakajiinamisha mbele yao; wakamkasirisha Bwana, akaghadhibika. Wakamwacha Bwana, wakamtumikia Baali na Maashtorethi.
Hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye ikawatia katika mikono ya watu waliowateka nyara, akawauza na kuwatia katika mikono ya adui ao pande zote; hata wasiweze tena kusimama mbele ya adui zao. Kila walikokwenda, mkono wa Bwana ulikuwa juu yao kuwatenda mabaya, kama Bwana alivyosema, na kama Bwana alivyowaapia; nao wakafadhaika sana.
Kisha Bwana akawainua waamuzi, waliowaokoa na mikono ya watu hao waliowateka nyara. Lakini nawakuwasikiliza hao waamuzi wao, maana walifanya uasherati kwa kuifuata miungu mingine wakajiinamisha mbele yao; wakageuka upesi, na kuiacha njia ile waliyoiendea baba zao, waliozitii amri za Bwana; bali wao hawakufanya hivyo. Na wakati Bwana alipowainulia waamuzi, ndipo Bwana alikuwa pamoja na mwamuzi huyo, akawaokoa na mikono ya adui zao siku zote za mwamuzi huyo; maana Bwana alighairi kwa ajili ya kuugua kwao kwa sababu ya watu wale waliowaonea na kuwasumbua.
Lakini ikawa, wakati alipokufa mwamuzi huyo, wakarudi nyuma wakafanya maovu kuliko baba zao. kwa kuifuata miungu mingine ili kuitumikia, na kuinama mbele yao; hawakuacha matendo yao, wala njia zao za ukaidi.
Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu
________
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 106: 34-37, 39-40, 43-44 (K) 4
(K) Ee Bwana, unikumbuke mimi,
kwa kibali uliyo nayo kwa watu wako.
Hawakuwaharibu watu wa nchi
Kama Bwana alivyowaambia;
Bali walijkhanganya na mataifa,
Wakajifunza matendo yao.(K)
Wakazitumikia sanamu zao,
Nazo zikawa mtego kwao.
Naam. walitoa wana wao na binti zao
Kuwa dhabihu kwa mashetani. (K)
Ndivyo walivyotiwa uchafu kwa kazi zao,
Wakafanya uasherati kwa matendo yao.
Hasira ya Bwana ikawaka juu ya watu wake,
Akauchukia urithi wake. (K)
Mara nyingi aliwaponya,
Bali walikuwa wakimwasi kwa mashauri yao,
Wakadhilika katika uovu wao.
Lakini aliyaangalia mateso yao,
Aliposikia kilio chao. (K)
________
SHANGILIO
1 Thes. 2:13
Aleluya, aleluya,
Lipokeeni neno la Mungu,
siyo kama neno la wanadamu,
bali kama neno la Mungu.
Aleluya
________
INJILI
Mt. 19: 16-22
Mtu mmoja alimwendea Yesu akamwambia, Mwalimu, nitende jambo gani jema, ili nipate uzima wa milele? Akamwambia, Kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja. Lakini ukitaka kuingia katika uzima, zishike amri. Akamwambia, Zipi? Yesu akasema, Ni hizi, Usiue, Usizini, Usiibe, Lsishuhudie uongo, Waheshimu baba yako na mama yako, na, Mpende jirani yako kama nafsi yako.
Yule kijana akamwambia, Haya yote nimeyashika; nimepungukiwa na nini tena? Yesu akamwambia, Ukitaka kuwa mkamilifu, enenda ukauze ulivyo navyo, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate. Yule kijana alipolisikia neno lile, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo
________
Copyright © 2025, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
Subscribe to:
Posts (Atom)