“ASALI
ITOKAYO MWAMBANI”
Jumamosi,
Desemba 19, 2021,
Juma
la 3 la Majilio
Yer.
23:5-8
Zab.
72:1-2, 12-13, 18-19 (K) 7
Mt.
1:18:24
Karibuni
sana wapendwa wa Bwana kwa adhimisho la misa takatifu asubuhi ya leo. Neno la
Bwana katika Zaburi ya wimbo wa katikati linatupatia matumaini ya ujio utakaoleta
furaha na amani milele. Mwenyehaki anatangazwa kwamba ndiye atakayesitawi na
kupata amani yake milele.
Mungu
ndiye mwenye uwezo wa kuleta amani na furaha kwa milele yote. Na kwa hakika
Zaburi hii ilikuwa utabiri wa ujio utakaokamilisha hili. Yesu ndiye ukamilifu
wa unabii huu.
Katika
somo la kwanza, Yeremia anatutangazia kwamba Yesu ndiye chipukizi toka katika
shina la Daudi, atakayetenda kwa hekima, na kutoa hukumu ya haki. Yuda
anayeonewa na mataifa ataokolewa. Nabii kwa hakika anaufurahia ujio huu kwa
namna ya pekee. Yesu ndiye ukamilifu wa yote yanayotangazwa na nabii leo.
Hivyo
tujifunze kumwamini Yesu. Kwa hakika yeye ndiye mfalme wetu, ndiye mwenye
kutupa faraja yetu, ndiye mwalimu wetu. Ulimwengu wote, viongozi wote wa
ulimwengu wanapaswa kujifunza toka kwa Yesu. Wajifunze kuwa watu wa haki na
kutawala kwa amani. Tabia za unganganiaji wa madaraka, ubinafsi na rushwa
vinaleta maumivu kwa wengi na vita duniani na yote haya ni kwa sababu tumekataa
kumwiga Yesu kama Mfalme na mwalimu wetu. Yesu ndiye mwalimu. Tujifunze kumtii
mfalme na mwalimu huyu.
Katika
somo la Injili, tunapata habari za kuzaliwa kwa Yesu. Kuzaliwa huku hakukuwa
rahisi sana kwani Yosefu na Maria walikuwa bado hawajapata uelewa wa kutosha
kuhusu kuzaliwa huku. Yosefu anakusudia kumwacha Maria kwa siri. Malaika wa
Mungu anamfumbulia Yosefu fumbo lililojificha kati yao na mwishowe Yosefu
anakubali kumpokea Yesu na Maria.
Sisi
tujifunze toka kwa Yosefu. Ukweli ni kwamba familia nyingi zina changamoto
lakini tujifunze kumsikiliza malaika wa Bwana ambaye huja na kusema nasi kila
siku akitufundisha namna ya kutatua hizo changamoto kama anavyomfundisha Yosefu
leo. Wengi wetu hatuisikilizi sauti ya Bwana kama alivyofanya Yosefu. Tunaenda
kuomba ushauri kwa watu wavijiweni na wanatupatia ushauri mmbaya na mwishowe
tunaharibu familia. Tuombe ushauri kwa watu wanaosali na waliokaribu na Bwana
hakika watatuongoza vyema. Tumsifu Yesu Kristo.
Copyright ©2013-2020 ©FurKat,
Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment