Tafakari
ya Kila siku
Ijumaa,
Oktoba 1, 2021,
Juma
la 26 la Mwaka
Bar
1: 15-22;
Ps
78: 1-5, 8-9;
Lk
10: 13-16
RUDI
KWA MUNGU!
Karibuni
ndugu zangu katika adhimisho la Ekaristi takatifu asubuhi ya leo. Neno la Bwana
asubuhi ya leo tunaanza kwa kuliangalia somo la kwanza linalotoka katika kitabu
cha Baruku. Hili somo la kwanza la leo ni sala ya Baruku aliyoiandika akiwa
utumwani Babuloni. Katika sala hii ambapo ndipo lilipo somo letu la kwanza,
Baruku anaungama kabisa kumwambia Mungu kwamba sisi ndio tuliofanya makosa,
hatukuzitii amri zako na ndiyo maana tumeishilia utumwani katika mateso haya.
Hivyo,
katika sala hii, anawatia moyo wale walioko utumwani kwamba mrudieni Bwana
jamani na kumwomba msamaha.
Fundisho
hili la kumrudia Bwana na kumwomba msamaha pia linasisitizwa na Yesu katika
injili ya leo. Yesu anaona kwamba miji ya Bestaida na korazini ilikuwa na
bahati ya kusikiliza na kuona miujiza ya Yesu lakini hawakubadilika. Hivyo
anawaambia kwamba wasipobadilika hakika watakiona cha moto.
Hili
ni fundisho kubwa sana kwetu ndugu zangu hasa sisi tunaohudhuria misa kila
siku. Yatupasa kuhakikisha kwamba tunakuwa mstari wa mbele katika kubadilika,
katika kuonesha kwamba wewe umeielewa injili, kwamba kuja kwako kanisani kila
siku kunakubadilisha-isije ikawa kwamba wewe kila siku unakuja kanisani,
unakomunika, umeingia katika vyama vyingi vya kitume-lakini ukitoka hapa
kanisani-nyumbani kwako au kazini kwako au mtaani kwako hakukaliki-kuko kama
Guantanamo.
Unanyanyasa
watu, vijana wako wa kazi, unawajibu watu vibaya, unatukana matusi-ukatili kila
kukicha-ukiguswa kidogo unanasa watu vibao kama mchezo. Nakwambia kama uko
hivyo, afadhali wale wasiokuja kanisani na adhabu yako itakuwa kubwa. Hivyo
ujio wetu kanisani utufanye tubadilike. Isije ikawa kwamba unakuja kanisani
kuja kuficha uovu. Tuishi Injili kwa matendo yetu na maneno yetu. Tukumbuke
maneno ya Mt.Fransisko wa Assisi kwamba "tuhubiri sana na inapobidi
tutumie maneno". Mt. Fransisko wa Assis atuombee katika sikukuu yake leo.
Nawatakia heri na baraka ndugu zangu wa mashirika ya Mt. Fransisko kwa sherehe
ya Baba yetu wa Kiserafi.
------------------------
Copyright ©2013-2020
©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment