Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

KRISTO NI NANI KWANGU?

 

“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”

Ijumaa, Septemba 24, 2021

Juma la 25 la Mwaka

 

 

Lk 9: 18-22

 

 

KRISTO NI NANI KWANGU?

 

Karibuni sana ndugu wapendwa kwa adhimisho la misa takatifu asubuhi ya leo. Neno la Bwana leo katika somo la kwanza Nabii anawatia moyo viongozi wa taifa la Yuda kwamba wasiogope ati watapata mali wapi ili waweze kulijenga hekalu la Bwana. Bwana ataagiza mali, na utukufu wote toka katika mataifa kuja kulijia hekalu la Yerusalemu na kulifanya lingae na kupambika kwani dhahabu ni ya Bwana, na kila utajiri uliopo kati ya mataifa ni mali ya Bwana pia. Hivyo Bwana aweza kuuchukua na kuuleta Yerusalem upambe hekalu lake.

 

Somo hili litufanye tuwe watu wenye kufanya bidiii zaidi tutambue kwamba tunapaswa kujitoa kwa ajili ya Bwana zaidi na zaidi ili kulifanya hekalu la Bwana lipendeze vyema. Hatupaswi kuogopa au kuona ugumu katika kumpatia Bwana kilichochake, Bwana apewe dhahabu na fedha yake, wapo wengi wamejidai kumnyima Bwana dhahabu na fedha yake bila kumtolea chochote lakini mwisho wa siku, wameviacha vitu hivi hapa ulimwenguni kwani vinabakia kuwa mali ya Bwana. Hivyo tukiwa hapa duniani, tukumbuke kuwa ni Mungu ameamua kutukabidhi ili tuvitunze. Tuache kujisahau na kufikiria kwamba ni vyetu. Hapana, tutaviacha hapa hapa.

 

Fedha na mali yote ni vya Bwana. Hivyo tusiache kumpa Bwana kilicho chake. Hata muda na vipaji tulivyonavyo ni kwamba tumekabidhiwa ili tumtunzie Bwana na ipo siku atavichukua. Na hivyo tusiishi kana kwamba ni vyetu na kwamba hatutakaa vichukuliwe toka kwetu. Hivyo tusisahau kutoa kwa ajili ya maskini kwa kila siku.

 

Katika somo la injili, Petro anamkiri Yesu waziwazi kwamba yeye ni masiha. Sisi tunapaswa kuwa kama Petro, yafaa tumkiri Yesu kuwa Kristo kwetu. Yesu kwa kila wakati anaigwa na wengi na hivyo waamini wanaoweweseka watashindwa kumtambua Yesu ni yupi. Wapo wanaofikiri kwamba yeye ni Yohane mbatizaji, wengine Elia na wengine ni mojawapo wa manabii. Na hawa watajitokeza hivihivi pia wakidai kwamba wao ni Yesu. Sisi tunapaswa kuwa makini, tukitambua kwamba Bwana Yesu kwa wakati wote wapo wanaotamani kumwiga, kuiga jina lake na ukuu wake. hivyo tumkiri Kristo kweli. Tuachane na matapeli.

 

 

 

------------------------

Copyright ©2013-2020 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

No comments:

Post a Comment