Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

MASOMO YA MISA, IJUMAA, AGOSTI 20, 2021

 

MASOMO YA MISA,

IJUMAA, AGOSTI 20, 2021

JUMA LA 20 LA MWAKA

________

 

SOMO I

Rut 1: 1, 3-6, 14-16, 22

 

Ikawa zamani za Waamuzi walipoamua, kulikuwa na njaa katika nchi. Akaondoka mtu mmoja wa Bethlehemu ya Yuda, akaenda kukaa katika nehi ya Moabu, yeye na mkewe na wanawe wawili. Akafa Elimeleki, mumewe Naomi; na yule mwanamke akasalia na wanawe wawili. Nao wakaoa wake katika wanawake wa Moabu; na jina la mmoja aliitwa Orpa, na jina la wa pili Ruthu. Wakakaa huko yapata miaka kumi. Wakafa na Maloni na Kilioni wote wawili; na huyo mwanamke akawa amefiwa na wanawe wawili, na mumewe pia.Ndipo alipoondoka, yeye na wakueze, ili kurudi kutoka nchi ya Moabu; maana huko katika nchi ya Moabu amesikia ya kwamba Bwana amewajilia watu wake na kuwapa chakula. Orpa akambusu mkwewe. akarejea kwa watu wake, lakini Ruthu akaambatana naye.

 

Naye akasema. Tazama. shemeji yako amerejea kwa watu wake, na kwa mungu wake; basi urejee wewe umfuate shemeji yake. Naye Ruthu akasema. Isinisihi nikuache, nirejee nisifuatane nawe; maana wewe uendako nitakwenda. na wewe ukaapo nitakaa. Watu wako watakuwa watu wangu, na Mungu wako atakuwa Mungu wangu.

 

Basi Naomi..akarudi; pamoja na Ruthu Mmoabi, mkwewe; ambao walirudi kutoka nchi ya Moabu; nao wakafika Bethlehemu mwanzo wa mavuno ya shayiri.

 

Neno la Bwana...Tumshukuru Mungu

________

 

WIMBO WA KATIKATI

Zab 146 : 5-10(K) 2

 

(K) Ee nafsi yangu, umsifu Bwana.

 

Heri ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake,

Na tumaini lake ni kwa Bwana, Mungu wake.

Aliyezifanya mbingu na nchi,

Bahari na vitu vyote vilivyomo. (K)

 

Huishika kweli milele,

Huwafanyia hukumu waliooncwa,

Huwapa wenye njaa chakula;

Bwana hufungua waliofungwa. (K)

 

Bwana huwafumbua macho waliopofuka;

Bwana huwainua walioinama;

Bw ana huwapenda wenye haki;

Bwana huwahifadhi wageni;

Huwategemeza yatima ya mjane. (K)

 

Bali njia ya wasio haki huipotosha.

Bwana atamiliki milele,

Mungu wako, Ec Sayuni. kizazi hata kizazi.

Aleluva. (K)

 

________

 

SHANGILIO

Zab 27:11

 

Aleluya, aleluya,

Ee Bwana, unifundishe njia yako,

na kuniongoza katika njia iliyonyoka.

Aleluya.

________

 

INJILI

Mt. 22: 34-40

 

Mafarisayo waliposikia ya kwamba amewafumba kinywa wale Masadukayo, walifanya shauri pamoja. Mmoja wao, mwana-sheria, akamwuliza, akimjaribu; Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu? Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote. Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza. Na yapili yafanana nayo, ni hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Katika amri hizi mbili hutegemea torati yote na manabii.

 

Neno la Bwana...Sifa kwako, ee Kristo

 

Copyright © 2020, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

No comments:

Post a Comment