MASOMO YA MISA JUNI 28,
2024
IJUMAA YA 12 YA
MWAKA
SOMO1
2 Fal 25: 1-12
Ikawa katika mwaka wa
kenda wa kutawala kwake, katika mwezi wa kumi, na siku ya kumi ya mwezi huo,
Nebukadreza, mfalme wa Babeli, akaja yeye na jeshi lake lote, kupigana na
Yerusalemu, akapanga hema zake kuukabili; bao wakajenga ngome juu yake pande
zote. Basi mji huo ulihusuriwa hata mwaka wa kumi na moja wa mfatae Sedekia.
Siku ya kenda ya mwezi wa nne njaa ilikuwa nzito ndani ya mji, hata hapakuwa na
chakula kwa watu wa nchi. Ndipo mahali pakabomolewa katika ukuta wa maji, watu
wote wa vita wakakimbia usiku kwa njia ya lango lililokuwa kati ya zile kuta
mbili, karibu na bustani ya mfalme; (basi wale Wakaldayo walikuwa wakiuzuia mji
pande zote;) mfalme akaenda kwa njia ya Araba. Lakini jeshi la Wakaldayo
wakamfuatia mfalme, wakampata katika nchi tambarare ya Yeriko; na jeshi lake
lote walikuwa wametawanyika na kumwacha. Ndipo wakamkamata mfalme, wakamchukua
kwa mfalme wa Babeli huko Ribla. wakatoa
hukumu juu yake. Wakawaua wana wa Sedekia mbele ya macho yake, wakampofusha
macho Sedekia, wakamfunga kwa pingu, wakamchukua mpaka Babeli.
Hata mwezi wa tano,
siku ya saba ya mwezi, ndio mwaka wa kumi na kenda wa mfalme Nebukadreza,
mfalme wa Babeli. Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, mtumishi wa mfalme wa
Babeli, akaingi Yerusalemu. Akaiteketeza nyumba ya Bwana, na nyumba ya mfalme;
na nyumba zote za Yerusalemu, naam, kila nyumba kubwa aliiteketeza kwa moto. Na
jeshi lote la Wakaldayo, waliokuwa pamoja na huyo amiri wa askari walinzi,
wakazibomoa kuta za Yerusalemu pande zote. Na mabaki ya watu waliosalia katika
mji, nao wale walioasi, na kumkimbilia mfalme wa Babeli, na mabaki ya watu wote
wengine, watu hao Nebuzaradani, amiri wa askari walinzi, akawachukua mateka.
Lakini huyo amiri wa askari walinizi akawaacha watu walio maskini ili wawe
watunza mizabibu na wakulima.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 137 : 1-6 (K). 6
(K) Ulimi wangu
ugandamane nisipokukumbuka.
Kando ya mito ya
Babeli ndiko tulikoketi,
Tukalia
tulipoikumbuka Sayuni.
Katika miti iliyo
katikati yake
Tulivitundika vinubi
vyetu. (K)
Maana huko
waliotuchukua mateka
Walitaka tuwaimbie;
Na waliotuonea
walitaka furaha;
Tuimbieni baadhi ya
nyimbo za Sayuni. (K)
Tuuimbeje wimbo wa
Bwana
Katika nchi ya ugeni?
Ee Ycrusalemu,
nikikusahau wewe,
Mkono wangu wa kuume
na usahau. (K)
Ulimi wangu na
ugandamane
Na kaakaa la kinywa
changu, nisipokukumbuka.
Nisipoikuza
Yerusalemu
Zaidi ya furaha yangu
iliyo kuu. (K)
SHANGILIO
Yn. 10:27
Aleluya, aleluya, Kondoo
wangu waisikia sauti yangu, nami nawajua, nao wanifuata. Aleluya.
INJILI
Mt. 8:1-4
Yesu aliposhuka mlimani, makutano mengi walimfuata. Na tazama, akaja mtu mwenye ukoma akamsujudia, akisema, Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa. Yesu akanyosha mkono, akamgusa, akisema, Nataka; takasika. Na mara ukoma wake ukatakasika. Yesu akamwambia, Angalia usimwambie mtu; ila enenda zako, ukajionyeshe kwa kuhani, ukaitoe sadaka kama alivyoamuru Musa, iwe ushuhuda kwao.
-------------------------
Copyright © 2024, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

No comments:
Post a Comment