Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

ASALI MUBASHARA-Jumatano 26/05/2021*

 *ASALI MUBASHARA-Jumatano 26/05/2021*


Karibuni ndugu zangu kwa adhimisho la misa takatifu asubuhi ya leo. Katika somo la kwanza tunaona sala ya wana wa IsraelI wakimuomba Mungu kwa unyoofu aoneshe nguvu zake juu ya mataifa yote. Lengo la sala hii wanatamani Mungu ajulikane kwa mataifa yote. Lakini sala hii pia inaomba ukumbozi wa mji wa Yerusalemu na watu wa Israeli kutoka katika mataifa mengine, ili Mungu awakusanye tena wakasujudu na kusali tena katika hekalu lao kama ilivyokuwa desturi yao. 


Ndugu zangu sala hii inatoa fundisho kwetu, tumejikuta tukitekwa na mawazo na mafundisho tofauti na mapenzi ya Mungu, kazi imetuteka, tumekuwa na tamaa ya mambo mengi na kwanamna hii, Mungu ameshindwa kutambulika kupitia sisi. Nasi tusali sala hii, tumuombe Mungu aturudishe tena kule tulikotawanyikia, aturudishe tena kwenye Yerusalemu zetu, kwenye ndoa yetu, kwenye familia zetu, kwenye upendo wetu na wenzetu, kwenye amani yetu. Tumetawanyika kwasababu ya chuki, ukosefu wa unyenyekevu, hatuwasadiki tena manabii wetu, viongozi wetu wa dini na mengine mengi. Tumuombe aturudishe ili tuweze tena kuwa wamoja. 


Apunguze ubabe wetu tuwe watumishi wa wenzetu na kuishi kwa amani.


Katika somo la Injili Yesu anawaonya wafuasi wake hasa kuhusu kupenda kuwatawala wenzao. Kupenda ukubwa badala ya utumishi. Yesu anapenda wafuasi wake watende kinyume kabisa na watawala wa dunia hii, wawatumikie watu wawaoshe miguu kama yeye alivyofanya. Wakae na maskini sio matajiri tuu. Wakae na wale waliopoteza matumaini katika jamanii.


Tuombe neema ya Mungu itusaidie nasi tuweze kuwapenda wenzetu na tujisikie furaha tunapo watumikia na sio tunapowatala. Tukapake dawa vidonda vyao sio kwenda kuviongezea majeraha. Wajisikie faraja kwa uwepo wetu. Nisikubali kusujudiwa nakuiba sifa za Mungu kwasababu tu mimi nikiongozi! Nitumikie nakujishusha zaidi na Mungu ajulikane kwa watu wote kwa utumishi wangu.



No comments:

Post a Comment