Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

KUKIMBILIA KWA YESU

 

“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”

Tafakari ya kila siku

Jumatatu, Februari 8, 2021.

Juma la 5 la Mwaka

 

Mwanzo 1: 1-19;

Zab 104: 1-2, 5-6, 10, 12, 24, 35;

Mk 6: 53-56.

 

KUKIMBILIA KWA YESU

 

Karibuni ndugu zangu kwa adhimisho la Misa Takatifu asubuhi ya leo. Neno la Bwana leo linatueleza kwamba Mwenyezi Mungu anaupenda ulimwengu, yeye ndiye aliyeuumba ulimwengu kwa nguvu ya neno lake, akapanga majira yote. Ndiye aliyeumba mito na vijito vyote. Dunia inapendeza kwa sababu yake. Tunamuomba azidi kuulinda ulimwengu wote.

Changamoto iliyopo ni mwanadamu kuharibu uumbaji na kwa ujanja ujanja wake. Anaingiza vitu visivyokuwa katika mpango wa Mungu. Anataka alete hata ndoa za jinsia moja. Anataka kuingiza hata matunda yanayozalishwa na kemikali na kupata ukubwa wa ajabu. Anacheza na uumbaji na kuzalisha vitu vya haraka haraka, kuku wa haraka haraka lakini vyote hivi vinauteketeza ulimwengu. Baadhi ya wanaume wameota matiti kutokana na kemikali zinazozalishwa na huyu mwanadamu anayeingilia uumbaji. Anadiriki hata kutengeneza mvua. Haya yote ni uchu wa mwanadamu kutaka kupata mali nyingi bila kujali afya ya wengine Uumaji wa Mungu tunauharibu. Tumwombe Mungu atufundishe kuutunza ulimwengu wake. Pia tumuombe atazame zile sehemu zinazotawaliwa na ukame na uchafu aziangalie kwa namna ya pekee.

Katika injili yetu, Yesu anawaponya wagonjwa mbalimbali. Injili ya leo inatuambia kwamba ni wale waliomgusa ndio tu walioponywa. Hivyo tukitaka uponyaji toka kwa Yesu, ni lazima tunyanyuke na kumgusa Yesu. Tusilale tukitegemea kuna atakayemgusa kwa ajili yetu. Tunyanyuke sisi wenyewe na kumgusa. Hata ukija kanisani, yabidi kunyanyuka sisi kama sisi na kumgusa, tusitegemee kwamba kuna anayemgusa kwa ajili yako. Kila mtu anakuja na shida yake. Hivyo lazima nimguse kwa namna ya pekee, nikutane naye. Usilale na kusema Mama/Baba au rafiki anasali kwa niaba yangu.

 

 

------------------------

Copyright ©2013-2020 ©FurKat, FurahayaKikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

No comments:

Post a Comment