
“KWARESIMA YA UKARIMU”
Tafakari ya Kwaresima
Alhamisi, Aprili 3, 2025.
Juma la 4 la Kwaresima
Kut 32: 7-14;
Zab 106: 19-23;
Yn 5: 31-47.
SALA ZINATUBADILI, TUNAKUWA VYOMBO VYA HURUMA
YA MUNGU!
Leo somo la kwanza linatuletea swali la
kushangaza. Mungu amekasirika, akiwa tayari kuwaangamiza Waisraeli kwasababu ya
kuabudu miungu mingine. Lakini Musa, anaongea naye kuhusu uamuzi wake. Tunaweza
kushangazwa inawezekana je Mungu wa milele asiye badilika abadili mawazo yake.
Ni kitu ambacho tunaweza tusielewe. Ambacho tunaweza kusema kwa ujasiri ni
kwamba Maandiko yanatupa ujumbe baada ya ujumbe ukielezea nguvu ya sala.
Abrahamu aliongea na Mungu ili asiangamize mji mzima, kama kutakuwa na watu
wachache wenye haki, je, kuna watu wachache kati yetu wanaoweza kusali kama
Abraham kwa Mungu?
Kazi alizozitenda Yesu zilimpa ushuhuda wa
utume aliopewa na Baba yake Mbinguni. Ujumbe wake uliongea na watu jinsi Baba
alivyo. Ushuhuda wake ulifunua kiini cha muunganiko wake na Mapenzi ya Baba.
Ingawaje miujiza yake ilikuwa ya hali ya juu kwa wote waliokuwa tayari
kumwamini, kazi alioifanya ya “pekee” ilikuwa juu ya unyenyekevu na upendo wa
kweli. Yesu alikuwa mwaminifu, mnyofu wa moyo kabisa. Kwahiyo, ushuhuda wa matendo
yake ya kawaida ya upendo, kujali, na kufundisha ndiyo yalio ziteka na kupata
mioyo ya watu wengi. Hata tendo dogo la Upendo liliongea mengi katika mioyo ya
watu.
Tutafakari leo, kama tupo tayari kufuata
mfano wa Musa na kuwa na muda wa kumfahamu Mungu na kuwa karibu kwa jinsi
anavyo tupenda sisi. Je tupo tayari kufungua mioyo yetu kwake ili tuweze kupata
huruma yake? Je, tupo tayari kwenda nje kwa wengine ambao hawana bahati kama
sisi, ili tuweze kugusa mioyo yao kwa moyo wa Kimungu, kwa kuangalia mahitaji
yao? Tutafakari pia wito wetu wakutoa ushuhuda wa Baba yetu wa Mbinguni,
kushirikisha upendo wa Baba kwa kila tunaye kutana naye. Kama tutakumbatia
utume huu, Injili itafunuliwa kwa wengine kupitia sisi, na mapenzi ya Mungu
yatafunuliwa na kutimia katika ulimwengu wetu.
Sala: Bwana, ninaomba niweze kuwa shahidi wa
upendo wako utokao moyoni mwako. Nipe neema niweze kuwa mkweli na mwaminifu.
Nisaidie mimi niweze kuwa chombo cha uhakika cha huruma ya moyo wako ili kazi
zangu zote zishuhudie huruma yako. Yesu, nakumini wewe. Amina.
No comments:
Post a Comment