
“KWARESIMA YA UKARIMU”
Tafakari ya Kwaresima
Jumatatu, Machi 17, 2025.
Juma la 2 la Kwaresima
Dan 9:4-10
Zab 79:8-11,13
Lk 6:36-38
USIHUKUMU!
Ulishawahi kukutana na mtu kwa mara ya kwanza na bila hata kuongea
na huyu mtu mara moja unahitimisha unayofikiri juu yake au wao? Kama sisi
wenyewe ni waaminifu ni lazima tukiri kwamba ni rahisi kuhukumu watu wengine
kwa haraka. Kilicho kigumu ni kubadilisha hukumu yetu tuliojiwekea kuhusu hao
wengine. Ni vigumu kuwahukumu tukiwapa mafanikio na kuondoa wasi wasi wetu na
kufikiri ni wazuri.
Yesu alivyosema “usihukumu nawe hauta hukumiwa” anatualika sisi
tusiwe watu wa kuwahukumu watu katika hali yeyote. Ulimwengu unahitaji watu
wengi wasio hukumu na wala kulaani. Tunahitaji watu wanao fahamu kutengeneza
urafiki na kuleta upendo usio na masharti. Na Mungu anataka wewe uwe mmoja wao
wa hao watu. Tutafakari ni mara ngapi tumekuwa watu wakuwahukumu watu, na
tutafakari ni kwa namna ghani sisi ni wazuri katika kutengeneza urafiki na wale
wote walio karibu yetu. Mwishowe, kama tumekuwa watu wa kutengeneza huu
urafiki, ni wazi tutapokea Baraka kutoka kwa wengine wanao tupatia na sisi
urafiki kama huo. Na kwa njia hiyo sisi wote tutabarikiwa.
Sala: Bwana, ninaomba unipe moyo usio hukumu. Ninaomba unisaidie
niwapende wote ninao kutana nao kwa mapendo matakatifu na kuwakubali. Ninaomba
unipe mapendo ya kweli na urafiki wa kweli kwa wengine ili niweze kuamini na
kufurahia upendo unaopenda mimi niwe nao. Yesu, nakuamini wewe. Amina.
No comments:
Post a Comment