
“KWARESIMA YA UKARIMU”
Tafakari ya Kwaresima
Alhamisi, Machi 13, 2025.
Juma la 1 la Kwaresima
Est 4:17, 23-25;
Zab 138:1-3, 7-8
Mt: 7:7-12
OMBENI NANYI MTAPEWA!
Mara baada ya kuwafundisha Wanafunzi wake kusali, leo Yesu
anawaambia: “ombeni nanyi mtapokea …” Baba yetu wa Mbinguni anatupatia kwa
neema zake yale yote tunayo muomba hata kwa jinsi tusio tegemea, na kwa wote
wanaojua na kutegemea upendo wake, husali kwa hakika. Sala inatokana na upendo
wetu kwa Mungu na upendo wake kwetu sisi. Hili linatusaidia kushirikisha upendo
wake kwa wengine, kwani Mungu amemimina upendo wake ndani ya Roho zetu kwa njia
ya Roho Mtakatifu. (Warumi 5: 5).
Yesu ana hakika kabisa kwamba tutakapo omba tutapokea, tutakapo
tafuta, tutapata, na tutakapo bisha hodi, tutafunguliwa mlango. Mara nyingi
tunaweza kuomba na kuomba, lakini tunaona sala zetu hazijibiwi, katika hali ya
jinsi tulivyo ziomba. Hili linaleta swali “sasa nisalije na nisali kwa ajili ya
nini?”. Lakini kila sala au ombi tunalosema linapaswa liwe kwa ajili ya mapenzi
ya Mungu yafanyike, hakuna zaidi, wala hakuna chakupunguza. Ni kwa ajili tu ya
mapenzi yake kamili yatimie.
Tutafakari leo, jinsi tunavyosali. Tubadili sala zetu ili ziwe
zinatafuta mambo mazuri ambayo Mungu anataka kuyaweka kwetu. Itakuwa ngumu mara
ya kwanza kuachana na mapenzi yetu na mawazo yetu, lakini mwishoni tutabarikiwa
na mambo mengi mazuri kutoka kwa Mungu.
Sala: Bwana, ninasali mapenzi yako yatimizwe katika kila kitu.
Ninatamani kukabidhi kwako, na kuamini mpango wako mkamilifu. Nisaidie Bwana
kuachana na mawazo yangu peke yangu na kutafuta ya kwako daima. Yesu, nakuamini
wewe. Amina.
No comments:
Post a Comment