Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

KUOMBA!




“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Kila siku
Alhamisi, Oktoba 10, 2024, 
Juma la 27 la Mwaka wa Kanisa

Gal 3: 1-5; 
Lk 1: 69-75; 
Lk 11: 5-13


KUOMBA!

“Ombeni nanyi mtapewa…” nimeomba mara nyingi, lakini sikupata hata kimoja. Haya ni majibu yetu kila mara kwenye huo ujumbe katika Injili. Lakini tujiulize, tunatulia nakujitafiti na kutafakari; je, nimeomba kwa ajili ya malengo sahihi? Je, ninafahamu thamani ya vitu ninavyo omba? Je, vitu ninavyo omba na kuhitaji nivya lazima kabisa? Mtoto asiye na meno anaweza kumuomba baba yake mua. Je, baba yake atampa? Hapana. Baba atasubiri mpaka akue awe na meno ndio ampe. 

Nyani hafahamu thamani ya dhahabu ulioshika. Lakini aweza kunyosha mkono kuomba, je utampatia? Hapana, haumpi. Kwasababu unafahamu thamani yake! Ni katika hali hiyo tunaweza tusijue tunanyoosha mkono kuomba nini, lakini Mungu anajua. Hii haimanishi tusiombe chochote tunacho penda. Tunaweza kuomba lakini kama hatuvipati tunavyo omba, tusikatishwe tamaa. Mungu anajibu katika hali ambayo itakunufaisha na njia ambayo itakufanya ulicho omba kisikutenge naye. 

Sala: Bwana, naomba mapenzi yako yatendeke. Amina

Copyright ©2013-2024 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

No comments:

Post a Comment