Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

KWA NINI YESU ANASALI?

John 17:9. Jesus Prays for You - Wellspring Christian Ministries


“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Pasaka
Alhamisi, Mei 16, 2024
Juma la 7 la Pasaka


Mdo 22: 30; 23: 6-11;
Zab 16: 1-2, 5-11 (K. 1);
Yn 17: 20-26


KWA NINI YESU ANASALI?


Leo tunamuona Yesu akituombea sisi tunao muamini. Ni bahati ilioje kuwa na Mungu anayetuombea? Ni furaha ilioje kuona tumepewa heshima kwa kutajwa ndani ya Injili na kuongelewa na Yesu? Yesu anawaombea wale watakao kuwa wafuasi wake baada ya kuwasikiliza mitume wake. Hapa sisi tupo kwani tunaamini waliotuachia mitume.

Wakati Yesu anavyo nyanyua macho yake mbinnguni, anasali kwa Baba yake wa mbinguni. Ukweli huu wa kunyanyua macho yake, unafunua jambo moja muhimu la uwepo wa Baba yake. Unafunua kwamba “Baba yupo juu ya yote”. Kwa hiyo kwa kuongea na Baba yake, Yesu anaonesha ishara hii kwa kumkiri kwamba Baba yupo juu ya yote. Tunapaswa pia kutambua uhusiano wa pekee na Yesu na Baba yake. Uhusiano wao ni uhsiano wa asili yote. 

Sala ya Yesu kwa Baba ilikuwa sisi wote ambao tutamwamini tuweze kushiriki umoja wa Baba na Mwana. Kwanza kwabisa tunaanza kwa kuona ukuu wa Mungu, kunyanyua macho yetu mbinguni na kuona ukweli, utukufu, ukuu, nguvu, na Mungu wa Majeshi. Tunapaswa kumuona Mungu huyu mtukufu na mkuu akishukia mioyo yetu, akiwasiliana na sisi, akitupenda sisi, akianzisha uhusiano wa karibu na sisi. Tunapaswa kukubali uwepo wake, kumwabundu akiwa anaisha ndani yetu, tukiongea naye na kumpenda yeye. 

Kitu cha kwanza anachoomba ni sisi tuwe na umoja (Yn 17: 21-23). Umoja wetu katika Mungu matokeo yake ni utume, kama Yesu anavyosema, “Ili ulimwengu utambue kuwa umenituma mimi” na tena “..ili ulimwengu uweze kutambua umenituma mimi na unawapenda wao kama unavyo nipenda mimi”. Zaidi na zaidi watu watakuwa na imani ndani ya Yesu, kwa uwepo wa Kanisa, na kudhihirisha kwa kutoa ushuhuda wa upendo wa Mungu ndani ya Kristo. 

Na tena Yesu anaendelea kusali “..na pia wao, ulionipa mimi, waweze kuwa nami pale nilipo, waweze kuona utukufu ulionipa, kwasababu ulinipenda mimi kabla ya kuwepo misingi ya ulimwengu.” Anaongelea maisha yetu yajayo katika maisha ya milele. Huko tutaona utukufu wake, usiofifia wala kuisha. Hapo tutakuwa naye, na tutamuona uso kwa uso.
Sala: Bwana, ninaomba unisaidie niweze kunyanyua macho yangu kuelekea mbinguni kwa sala. Ninakuomba nikugeukie wewe na Baba. Katika sala hiyo naomba nitambue kuwa upo wazi katika moyo wangu ambapo una abudiwa na kupendwa. Yesu, ninakuamini wewe. Amina.

Copyright ©2013-2024 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

No comments:

Post a Comment