SIKU YA TISA: JUMAMOSI BAADA
YA PASAKA
NAMNA YA KUFANYA NOVENA KWA
HURUMA YA MUNGU
Sala ya kutubu:
Mungu wangu, ninatubu sana dhambi
zangu, kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza, wachukizwa na dhambi, basi
sitaki kukosa tena, nitafanya kitubio, naomba neema yako nipate kurudi kwako,
Amina.
Nia ya sala za leo:
SIKU YA TISA
Maneno ya Mwokozi wetu: “Leo niletee roho za wale waliokwishaingia hali ya
uvuguvugu, na uwazamishe katika kilindi cha Huruma yangu. Roho hizi huumiza
sana Moyo wangu. Roho yangu iliteseka sana kwa kinyaa cha kutisha kule
bustanini kwa sababu ya roho hizi vuguvugu. Ni wao waliosababisha nilie; Baba
ikiwa ni mapenzi yako uniondolee mbali kikombe hiki nisikinywe. Kwa watu hawa,
tumaini la mwisho lililowabakia ni kuikimbilia Huruma yangu tu basi”.
Tuwaombee watu walio na hali ya uvuguvugu, hali ya hatari
kwa wokovu, ambao walisababisha mateso makali sana kwa Yesu Kristu kule
bustanini mwa mizeituni.
W: Ee Yesu
mwenye Huruma nyingi, Wewe u Huruma yenyewe, Uzipokee roho vuguvugu ndani ya
Moyo wako ulio na Huruma bila kiasi. Roho hizi ni kama mizoga iliyojaa na
kunuka uvundo, uziingize katika moto wa upendo wako safi, zitakasike. Roho hizi
zilikutia kinyaa kingi. Sasa uziwashe tena, na kwa Huruma yako, uzipe paji la
Upendo Mtakatifu. Ee Yesu mwenye Huruma Kuu, tumia uwezo wako na uzipatie roho
hizi bidii tena, kwani kwako hakuna kitu kisichowezekana, na kwa njia hii
wapate kuitukuza daima Huruma Yako. Amina.
Baba yetu, Salamu Maria
………..Atukuzwe,
W: Baba wa Huruma, uzitazame kwa macho ya Huruma, roho zilizo
vuguvugu, ambazo katika hali yao hiyo, wameingizwa ndani ya Moyo wa Mwanao
Yesu, ulio kilindi cha Huruma. Ee Baba wa Huruma, tunakusihi kwa ajili ya
mateso makali ya Mwanao Mpenzi, Bwana wetu Yesu Kristu, uliyovumilia pale
msalabani, kwa masaa matatu ukiwa katika hali ya umahututi ya uchungu,
uziwezeshe hata roho hizi zipupie utukufu wako. Uijaze mioyo ya watu hawa
upendo wa kweli, hivyo kwa Baraka takatifu, waweze kutenda matendo mengi ya
huruma hapa duniani, na huko Mbinguni wafike kuitukuza Huruma yako Kuu kwa
milele yote. Amina.
Rozari ya Huruma ya Mungu
(Tumia chembe za rozari ya kawaida)
Baba yetu
… Salamu Maria …. x3
Nasadiki kwa Mungu Baba Mwenyezi …….
Kwenye chembe kubwa
Baba wa Milele, ninakutolea
Mwili na Damu, Roho na Umungu, wa Mwanao Mpenzi sana, Bwana wetu Yesu Kristu,
kwa ajili ya malipizi ya dhambi zetu, na dhambi za dunia nzima.
kwenye chembe ndogo
Mwanzishaji: Kwa ajili ya mateso
makali ya Bwana wetu Yesu Kristo,
Wote huitika: Utuhurumie sisi na dunia nzima.
Mwisho wa Rozari sali mara
tatu sala ifuatayo:
Mungu Mtakatifu, Mtakatifu
mwenye Enzi, Mtakatifu unayeishi milele, Utuhurumie sisi na dunia nzima.
Litania ya Huruma ya Mungu
No comments:
Post a Comment