NOVENA YA HURUMA YA MUNGU
SIKU YA TANO: JUMANNE BAADA YA
PASAKA
NAMNA YA KUFANYA NOVENA KWA
HURUMA YA MUNGU
Sala ya kutubu:
Mungu wangu, ninatubu sana dhambi
zangu, kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza, wachukizwa na dhambi, basi
sitaki kukosa tena, nitafanya kitubio, naomba neema yako nipate kurudi kwako,
Amina.
Nia ya sala za leo:
SIKU YA TANO
Maneno ya Mkombozi: “Leo niletee roho za ndugu waliojitenga na Kanisa, na uwazamishe katika
Bahari Kuu ya Huruma yangu. Wakati ule wa mateso yangu makali, watu hawa
waliurarua mwili wangu na roho yangu, yaani Kanisa langu. Pindi warudipo tena
katika Umoja wa Kanisa, majeraha yangu hupona, na kwa njia hii wanapunguza
ukali wa mateso yangu”.
Tuwaombee wale waliopotoka
katika Imani Katoliki na kujitenga na Kanisa.
W. Ee Yesu Mpole na mwenye Huruma, Wewe u Huruma na Wema wenyewe, hukatai
kuwapa mwanga wale wote wanaoutafuta. Uzipokee ndani ya Moyo wako wenye Huruma,
roho za ndugu zetu waliojitenga. Uwavute kwa mwanga wako, ili warudi tena
katika Umoja wa Kanisa lako Takatifu, na uwadumishe humo, wasiweze kutoroka
tena Moyo wako wenye Huruma sana, bali uwawezeshe wao pia pamoja nasi, kuusifu
na kuutukuza ukarimu wa Huruma Yako Kuu, kwa milele na milele. Amina.
Baba yetu ……. Salamu Maria ……..
Atukuzwe …………..
W. Baba wa Milele, uzielekee kwa macho ya huruma, roho za ndugu zetu
waliojitenga na Kanisa lako Takatifu, hasa wale waliozitapanya Baraka zako na
kuzitumia vibaya neema zako, kwa kuendelea kishupavu katika mafundisho yao ya
upotofu. Usiyaangalie hayo makosa yao, bali uutazame upendo wa Mwanao Mpenzi,
pamoja na mateso yake makali aliyovumilia kwa ajili yao. Watu hawa pia,
wameingizwa ndani ya Moyo wa Yesu Mwanao, wenye Huruma Kuu. Uwawezeshe vile
kwamba, wao pamoja na sisi sote, tuisifu na kuitukuza Huruma Yako Kuu, kwa
milele na milele. Amina.
Rozari ya Huruma ya
Mungu
(Tumia chembe za rozari ya
kawaida)
Baba yetu
… Salamu Maria ….
x3 Nasadiki
kwa Mungu Baba Mwenyezi …….
Kwenye chembe kubwa
Baba wa Milele, ninakutolea
Mwili na Damu, Roho na Umungu, wa Mwanao Mpenzi sana, Bwana wetu Yesu Kristu,
kwa ajili ya malipizi ya dhambi zetu, na dhambi za dunia nzima.
kwenye chembe ndogo
Mwanzishaji: Kwa ajili ya mateso
makali ya Bwana wetu Yesu Kristo,
Wote huitika: Utuhurumie sisi na dunia nzima.
Mwisho wa Rozari sali mara
tatu sala ifuatayo:
Mungu Mtakatifu, Mtakatifu
mwenye Enzi, Mtakatifu unayeishi milele, Utuhurumie sisi na dunia nzima.
Litania ya Huruma ya Mungu
No comments:
Post a Comment