NOVENA YA HURUMA YA MUNGU
SIKU YA SITA: JUMATANO BAADA
YA PASAKA
NAMNA YA KUFANYA NOVENA KWA
HURUMA YA MUNGU
Sala ya kutubu:
Mungu wangu, ninatubu sana dhambi
zangu, kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza, wachukizwa na dhambi, basi
sitaki kukosa tena, nitafanya kitubio, naomba neema yako nipate kurudi kwako,
Amina.
Nia ya sala za leo:
SIKU YA SITA
Maneno ya Mwokozi wetu: “Leo niletee roho za watu walio wapole na wanyenyekevu wa moyo, pamoja na
roho za watoto wadogo, na uzizamishe katika kilindi cha Huruma yangu. Roho hizi
hufanana kwa ukaribu zaidi na Moyo wangu. Watu hawa ndio walionitia nguvu
wakati wa mateso na uchungu wa mahututi yangu. Niliwaona kama malaika wa duniani,
ambao watakesha daima kuabudu katika altare zangu. Kwa mafuriko yangu,
nitawamwagia neema zangu zote, kwa maana ni roho ile tu iliyo na unyenyekevu
inaweza kupata neema zangu. Ninawapendelea watu walio wanyenyekevu na kuwaamini
sana.”
Tuwaombee watoto wadogo pamoja
na roho zile zenye unyofu kama wao.
W. Ee Yesu
mwenye Huruma sana, Wewe Mwenyewe ulisema: “Jifunzeni kwangu kwa maana Mimi ni
mpole na mnyenyekevu wa Moyo”, uwapokee ndani ya Moyo wako uliojaa Huruma, watu
wote walio wapole na wanyenyekevu, pamoja na roho za watoto wadogo. Roho hizi
hustaajabisha Mbingu nzima, maana wanapotokea mbele ya Kiti cha Enzi cha Baba
wa mbinguni, huwa kama shada la maua litoalo harufu tamu ya marhamu safi, na
kuifurahisha Mbingu nzima. Mungu Mwenyewe hufurahia manukato yao safi. Roho
hizi zina makao ya daima ndani ya Moyo wako wenye Huruma ee Yesu. Na daima hukuimbia wimbo wa
Huruma na Upendo wako. Amina.
Baba yetu …… Salamu Maria ……..
Atukuzwe …….
W. Baba wa Milele, uzitazame kwa macho ya Huruma, roho za watu wote walio
wapole na wanyenyekevu wa moyo, pamoja na roho za watoto wadogo, walioingizwa
katika makao ambayo ni Moyo wa Yesu Mpenzi, ulio na Huruma nyingi. Roho za watu
hawa, hufanana na Mwanao kwa kwa karibu zaidi. Harufu yao tamu ya fadhila
hukufurahisha sana, nayo hupanda ikianzia hapa duniani mpaka kwenye Kiti chako
Kitukufu. Ee Baba wa Huruma na wema wote, ninakuomba, kwa ule upendo ulio nao
kwa roho hizi penzi, na kwa ajili ya furaha uipatayo kwao, utubariki sisi na
dunia nzima, ili sote pamoja tuungane katika kuisifu Huruma Yako, kwa milele
yote. Amina.
Rozari ya Huruma ya
Mungu
(Tumia chembe za rozari ya
kawaida)
Baba yetu
… Salamu Maria ….
x3 Nasadiki
kwa Mungu Baba Mwenyezi …….
Kwenye chembe kubwa
Baba wa Milele, ninakutolea Mwili
na Damu, Roho na Umungu, wa Mwanao Mpenzi sana, Bwana wetu Yesu Kristu, kwa
ajili ya malipizi ya dhambi zetu, na dhambi za dunia nzima.
kwenye chembe ndogo
Mwanzishaji: Kwa ajili ya mateso
makali ya Bwana wetu Yesu Kristo,
Wote huitika: Utuhurumie sisi na dunia nzima.
Mwisho wa Rozari sali mara
tatu sala ifuatayo:
Mungu Mtakatifu, Mtakatifu
mwenye Enzi, Mtakatifu unayeishi milele, Utuhurumie sisi na dunia nzima.
Litania ya Huruma ya Mungu
No comments:
Post a Comment