Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

MASOMO YA MISA, JUMAPILI, APRILI 21, 2024


MASOMO YA MISA, JUMAPILI, APRILI 21, 2024
DOMINIKA YA 4 YA PASAKA, MWAKA B

SOMO  1
 Mdo.4:8-12

Ndipo Petro, akijaa Roho Mtakatifu, akawaambia, Enyi wakubwa wa watu na wazee wa Israeli, kama tukiulizwa leo habari ya jambo jema alilofanyiwa yule mtu dhaifu, jinsi alivyoponywa, jueni ninyi nyote na watu wote wa Israeli ya kuwa kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye ninyi mlimsulibisha, na Mungu akamfufua katika wafu, kwa jina hilo mtu huyu anasimama ali mzima mbele yenu. Yeye ndiye jiwe lile lililodharauliwa na ninyi waashi, nalo limewekwa kuwa jiwe kuu la pembeni. Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.

Neno la Bwana......................................Tumshukuru Mungu.


WIMBO WA KATIKATI
Zab 118:1,8-9,21-23,26,28-29

(K)Jiwe walilolikataa waashi, Limekuwa jiwe kuu la pembeni

Aleluya. 
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, 
Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Ni heri kumkimbilia Bwana 
Kuliko kuwatumainia wanadamu.
Ni heri kumkimbilia BWANA. 
Kuliko kuwatumainia wakuu.

Nitakushukuru kwa maana umenijibu,
Nawe umekuwa wokovu wangu.
Jiwe walilolikataa waashi 
Limekuwa jiwe kuu la pembeni.
Neno hili limetoka kwa Bwana, 
Nalo ni ajabu machoni petu.

Na abarikiwe yeye ajaye kwa jina la Bwana; 
Tumewabarikia toka nyumbani mwa Bwana
Ndiwe Mungu wangu, nami nitakushukuru, 
Ndiwe Mungu wangu, nami nitakutukuza.
Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema, 
Kwa maana fadhili zake ni za milele.


SOMO  2
1Yoh.3:1-2

Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye. Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona kama alivyo.

Neno la Bwana........................................Tumshukuru Mungu. 


Shangilio
Yn 10:14

Aleluya aleluya
Mimi ndimi mchungaji mwema;
nao walio wangu nawajua;
Nao walio wangu wanijua mimi . 
Aleluya


Injili
Yn.10:11-18

Siku ile,Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo. Mtu wa mshahara, wala si mchungaji, ambaye kondoo si mali yake, humwona mbwa-mwitu anakuja, akawaacha kondoo na kukimbia; na mbwa-mwitu huwakamata na kuwatawanya. Yule hukimbia kwa kuwa ni mtu wa mshahara; wala mambo ya kondoo si kitu kwake. kama vile Baba anijuavyo, nami nimjuavyo Baba. Nami nautoa uhai wangu kwa ajili ya kondoo. Ndiposa Baba anipenda, kwa sababu nautoa uhai wangu ili niutwae tena. Hakuna mtu aniondoleaye, bali mimi nautoa mwenyewe. Nami ninao uweza wa kuutoa, ninao na uweza wa kuutwaa tena. Agizo hilo nalilipokea kwa Baba yangu.

Neno la Bwana...........Sifa kwao Ee Kristo. 


Copyright © 2024, "MASOMO YA MISA" published by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania. Readings reproduced by Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

No comments:

Post a Comment