“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Kila siku
Ijumaa, Oktoba 13, 2023,
Juma la 27 la Mwaka
Gal 3:7-14
Zab 111:1-6 (K) 5
Lk 11: 15-26
KUTAMBUA NGUVU YA MUNGU
Yesu alikataliwa na kulaaniwa na baadhi ya watu. Lakini kuna kila sababu na
vithibitisho kwamba Yeye ndiye ajaye. Wakati Yesu alipo samehe dhambi za yule
mtu aliyepooza viongozi wa Wayahudi walimlaani Yesu kwa kukufuru Mungu, na
baada ya yule mwanamke mdhambi kumpangusa Yesu kwa nywele zake na kumpaka
mafuta Mafarisayo walimlaumuYesu kwanini anamruhusu amguse. Wakati Yesu alivyo
mtoa pepo yule mtu aliye kuwa amepagawa na pepo watu walionesha mioyo migumu.
Leo katika somo la Injili Yesu anasema “kama ni kwa kidole cha Mungu natoa
pepo, mjue kwamba ufalme wa Mungu umeshakuja kati yenu”. Yesu anasema hivi
kujulisha watu kwamba Masiha ameshakuja kati yao.
• Ufalme na nyumba-Yeye ni Ufalme mwingine na tofauti na nyumba ya muovu.
• Mtoa Pepo-alihitahi kuheshiwa angalao basi kama viongozi wengine.
• Kidole cha Mungu-Yeye ana nguvu zote.
• Mtu mwenye nguvu. Yeye ana nguvu kuliko shetani.
• Nyumba iliyo tupu-alipenda kila mtu asafishe nyumba yake ili yeye aje
akae na kujaza neema.
Je, tunajibuje katika alama ya Mkono wa ukomozi wa Mungu katika maisha yetu
na katika maisha ya wengine? Kazi ya ukombozi ya Mungu inahitaji ushirikiano
kutoka kwetu. Je, tupo tayari kumgeukia Bwana na kuamini?
Sala: Baba, tufundishe kutambua nguvu yako na kazi yako katika ulimwengu
huu na kukugeukia kwa Imani. Yesu, nakuamini wewe.
Copyright ©2013-2024 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see
www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment