Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

KUTAMBUA NGUVU YA MUNGU



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Tafakari ya Kila siku
Ijumaa, Oktoba 13, 2023,
Juma la 27 la Mwaka

Gal 3:7-14
Zab 111:1-6 (K) 5
Lk 11: 15-26


KUTAMBUA NGUVU YA MUNGU


Yesu alikataliwa na kulaaniwa na baadhi ya watu. Lakini kuna kila sababu na vithibitisho kwamba Yeye ndiye ajaye. Wakati Yesu alipo samehe dhambi za yule mtu aliyepooza viongozi wa Wayahudi walimlaani Yesu kwa kukufuru Mungu, na baada ya yule mwanamke mdhambi kumpangusa Yesu kwa nywele zake na kumpaka mafuta Mafarisayo walimlaumuYesu kwanini anamruhusu amguse. Wakati Yesu alivyo mtoa pepo yule mtu aliye kuwa amepagawa na pepo watu walionesha mioyo migumu.

Leo katika somo la Injili Yesu anasema “kama ni kwa kidole cha Mungu natoa pepo, mjue kwamba ufalme wa Mungu umeshakuja kati yenu”. Yesu anasema hivi kujulisha watu kwamba Masiha ameshakuja kati yao.

• Ufalme na nyumba-Yeye ni Ufalme mwingine na tofauti na nyumba ya muovu.
• Mtoa Pepo-alihitahi kuheshiwa angalao basi kama viongozi wengine.
• Kidole cha Mungu-Yeye ana nguvu zote.
• Mtu mwenye nguvu. Yeye ana nguvu kuliko shetani.
• Nyumba iliyo tupu-alipenda kila mtu asafishe nyumba yake ili yeye aje akae na kujaza neema.

Je, tunajibuje katika alama ya Mkono wa ukomozi wa Mungu katika maisha yetu na katika maisha ya wengine? Kazi ya ukombozi ya Mungu inahitaji ushirikiano kutoka kwetu. Je, tupo tayari kumgeukia Bwana na kuamini?

Sala: Baba, tufundishe kutambua nguvu yako na kazi yako katika ulimwengu huu na kukugeukia kwa Imani. Yesu, nakuamini wewe.



Copyright ©2013-2024 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

No comments:

Post a Comment