Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

KUFANYWA UPYA KWA NJIA YA KRISTO!


“KUFUFUKA NA KRISTO”
Tafakari ya Pasaka
Jumapili, Aprili 9, 2023

VIGILIA YA PASAKA

Mwa 1:1-2:2, Zab 103:1-2,5-6,10,12-14,24,35 au Zab 32:4-7,12-13,20,22;
Mwa 22:1-18, Zab 15:5,8-11;
Kut 14:15-15:1, Kut 15;
Isa 54:5-14 Zab 29:2,4-5,11-13;
Isa 55:1-11, Is 12;
Bar 3:9-15,32-4:4, Zab 18:8-11;
Ez 36:16-28, Zab 41:2-3,5,42:3-4 au Zab 50:12-15,18-19;
Rom 6:3-11, Zab 117:1-2,16-17,22-23;
Mt 28:1-10.


KUFANYWA UPYA KWA NJIA YA KRISTO!


Liturjia ya leo inatualikwa kwenye mafumbo ya uumbaji mpya. Moto mpya unawasha na mshumaa mpya wa Pasaka unawashwa. Kanisa linasogea kutoka kwenye giza kuelekea kwenye mwanga tunavyo washa mishumaa yetu kutoka katika moto huu. Maji mapya yanabarikiwa na kwa maji hayo waumini wapya wanaingia katika kanisa kwa njia ya ubatizo. Ndio, Yesu anafanya mambo yote mapya.

Maadhimisho yana anza wakati taa zote zikiwa zimezimwa. Padre anabariki moto na kuandaa mshumaa wa Pasaka. Moto unatumika kuwasha mshumaa unaotumika kama mwanga alama ya Yesu. Mwanga umetajwa katika Biblia katika msatari wa tatu wa sura ya kwanza ya kitabu cha Mwanzo: Mungu anasema “na kuwe na Mwanga”. Kabla ya hili mwandishi anaonesha uwepo wa giza kubwa linalotisha. Mshumaa wa Pasaka unatukumbusha sisi kuhusu Mwanga. Sisi wote tumetembea katika giza Isaya anasema 9:2. Mioyo yetu ilivyokuwa katika giza ilikwama (Yn 11:10). Hatukujua tuende wapi wala tupo wapi hadi tukaanguka kwenye dhambi.

Yesu, Mwanga wa ulimwengu (Yn 9:5) alikuja ulimwenguni kuja kuuangaza ubinadamu wetu (Yn 1:4) na bado wakakataa mwanga huu na watu wakapenda mno giza (Yn 3:19). Usiku huu wa Pasaka unatukumbusha kuhusu hili. Jengo la Kanisa lipo katika giza. Tupo gizani kama hatuna Kristo. Licha ya hili giza kubwa mwanga mdogo wa mshumaa huu wa Pasaka unauwezo wa kutuangaza nasi tukaona mlango wa kuingia kanisani. Mwanga huu mdogo unatusaidia kuingia bila kujikwaa. Watu walivyo washa mishumaa wao kutoka katika mshumaa wa Pasaka, mwanga umeangaza zaidi na zaidi tukaanza kuona nyuso za kila mmoja wetu. Mwanga wa Kristo unafufua sura ya Mungu ndani yetu. Mwanga tunaopokea haupaswi kufichika, na wala hatupaswi kuanguka kwenye giza, kwani sisi sasa tumekuwa watoto wa mwanga (1 Thes 5:5).

Tunapaswa kwenda ulimwenguni na kuangazia kama nyota ya mbinguni inavyo angaza kwenye anga. Licha ya kuwa ndogo kwa muonekano inangaa kati ya giza kubwa lililopo angani. Maisha yetu ya Ukristo yanapaswa kuwa shahidi wa Kristo. Mwanga wetu tunaopokea kwa Kristo haupaswi kungara sana kiasi cha kuwaumiza wengine. Na wala haupaswi kuwachoma kiasi cha kuwaachia makovu. Tunapaswa kuwa wanyenyekevu na kuwakilisha mwanga wa Kristo kwa mapendo. Yesu ni mwanga unaoendelea kungaa katika ulimwengu huu wa giza. Amefufuka na yupo pamoja nasi na atakuja siku ya mwisho. Tutumie muda wetu tukiwa hapa duniani kwa kuleta mwanga wa Kristo ulimwenguni.

Yesu anaumba upya ulimwengu uliokuwa umeanguka na kuharibiwa na dhambi na anatuumba upya kila mmoja wetu. Analeta uponyaji na utakatifu katika maisha yetu. Hatuwekei viraka bali anatufanya wapya kabisa. Tunamuomba yeye atujaze na furaha za ukombozi wake. Tunamuomba aweke wimbo mpya mioyoni mwetu. Wewe ni kiumbe kipya.

Sala: Bwana nifanye mpya: nijaze na mwanga wako na fukuza giza ndani mwangu. Nitoe katika kifo na kunipeleka katika uhai, kutoka katika mtafaruku na kuniweka kwenye njia njema, kutoka katika giza kwenda kwenye mwanga. Yesu, nakuamini wewe. Amina

TUNAWATAKIA HERI YA PASAKA WASOMAJI WA TAFAKARI ZETU NA MARAFIKI WOTE -Furaha ya Kikatoliki- KRISTO AWAANGAZEE. AMINA


Copyright ©2013-2023 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

No comments:

Post a Comment