MASOMO YA MISA, DESEMBA 12, 2022
JUMATATU, JUMA LA 3 LA MAJILIO
Kumbukumbu ya Bikira Maria wa Guadalupe
SOMO 1
Hes 24:2-7.15-17
Siku zile Balaamu aliinua macho yake akawaona Israeli,
wamekaa kabila; roho ya Mungu ikamjia. Akatunga mithali yake akasema, Balaamu
macho asema, Yule mtu aliyefumbwa macho asema; asema, yeyey asikiaye maneno ya
Mungu, yeye aonaye maono ya Mwenyezi, akianguka kifudifudi, amefumbulia macho;
mahema yako ni mazuri namna gani, ee Yakobo, maskani zako, ee Israeli! Mfano wa
bonde zimetandwa, mfano wa bustani kando yam to, mfano wa mishubiri aliyoipanda
Bwana, mfano wa mierezi kando ya maji. Maji yatafurika katika ndoo zake, na
mbegu zake zitakuwa katika maji mengi. Na mfalme wake atadhimishwa kuliko
Agagi, na ufalme wake utatukuzwa.
Akatunga mithali yake akasema, Balaamu mwana wa Beori
asema, yule mtu aliyefumbwa macho asema, yeyey asikiaye maneno ya Mungu, na kuyajua
maarifa yake Aliye Juu. Yeyey aonaye maono ya Mwenyezi, akianguka kifudifudi,
amefumbuliwa macho, namwona, lakini si sasa; namtazama, lakini si karibu; nyota
itatokea katika Yakobo; na fimbo ya enzi itainuka katika Israeli.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 25:4 – 6, 7b – 9 (K) 4
(K) Ee Bwana unijulishe njia zako.
Ee Bwana, unijulishe njia zako,
Unifundishe mapito yako,
Uniongoze katika kweli yako,
Na kunifundisha. (K)
Ee Bwana, kumbuka rehema zako na fadhili zako,
Maana zimekuwako tokea zamani.
Unikumbuke kwa kadiri ya fadhili zako,
Ee Bwana kwa ajili ya wema wako. (K)
Bwana yu mwema, mwenye adili,
Kwa hiyo atawafundisha wenye dhambi njia.
Wenye upole akawaongoza katika hukumu,
Wenye upole atawafundisha njia yake. (K)
SHANGILIO
Zab. 85:7
Aleluya, aleluya,
Ee Bwana, utuonyeshe rehema zako, utupe wokovu wako.
Aleluya.
INJILI
Mt. 21:23 – 27
Siku ile Yesu alipokwisha kuingia hekaluni, wakuu wa
makuhani na wazee wa watu wakamwendea alipokuwa akifundisha, wakasema, Ni kwa
amri gani unatenda mambo haya? Naye ni nani aliyekupa amri hii? Yesu akajibu,
akawaambia, Na mimi nitawauliza neno moja; ambalo mkinijibu, nami nitawaaambia
ni kwa amri gani ninatenda haya. Ubatizo wa Yohana ulitoka wapi? Ulitoka
mbinguni, au kwa wanadamu?
Wakahojiana wao kwa wao, wakisema, Tukisema, Ulitoka
mbinguni, atatuambia, Mona basi hamkumwamini? Na tukisema, Ulitoka kwa wanadamu,
twaogopa mkutano; maana watu wote wamwona Yohana kuwa ni nabii. Wakamjibu Yesu
wakasema, Hatujui. Naye akawaambia, Wala mimi siwaambii ninyi ni kwa amri gani
ninatenda haya.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo
Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA
MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright ©
1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of
Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha
ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment