MASOMO YA MISA, NOVEMBA 24, 2022
ALHAMISI, JUMA LA 34 LA MWAKA WA KANISA
KUMBUKUMBU YA WATAKATIFU ANDREA DUNG-LAC NA WENZAKE
SOMO 1
Ufu. 18:1 – 2, 21 – 23; 19:1 – 3, 9
Mimi, Yohane, naliona malaika mwingine, akishuka kutoka
mbinguni, mwenye mamlaka kuu; na nchi ikaangazwa kwa utukufu wake. Akalia kwa
sauti kuu, akisema, Umeanguka, umeanguka Babeli ule mkuu; umekuwa maskani ya
mashetani, na ngome ya kila roho mchafu, na ngome ya kila ndege mchafu mwenye
kuchukiza.
Na malaika mmoja mwenye nguvu akainua jiwe, kama jiwe
kubwa la kusagia, akalitupa katika bahari, akisema, Kama hivi, kwa nguvu
nyingi, utatupwa Babeli, mji ule mkuu, wal ahautaonekana tena kabisa. Wala
sauti ya wapiga vinanda, na ya wapiga zomari, nay a wapiga filimbi, nay a
wapiga baragumu, haitasikiwa ndani yako tena kabisa; wala fundi awaye yote wa
kazi yoyote hataonekana ndani yako tena kabisa; wal asauti ya jiwe la kusagia
haitasikiwa ndani yako tena kabisa; wal anuru ya taa haitamulika ndani yako
tena kabisa; wala sauti ya bwana arusi na bibi arusi haitasikiwa ndani yako tena
kabisa; maana hao wafanya biashara wako walikuwa wakuu wa nchi, kwa kuwa
mataifa yote walidanganywa kwa uchawi wako.
Baada ya hayo nikasikia sauti kama sauti ya makutano
mengi, sauti kubwa mbinguni, ikisema, Aleluya; Wokovu na utukufu na nguvu zina
Bwana mungu wetu; kwa kuwa hukumu zake ni za kweli na za haki; maana amemhukumu
yule kahaba mkuu aliyeiharibu nchi kwa uasherati wake, na kuipatiliza damu ya
watumwa wake mkononi mwake. Wakasema mara ya pili, Aleluya. Na moshi wake hupaa
juu hata milele na milele.
Naye akaniambia, Andika, Heri walioalikwa karamu ya arusi
ya Mwanakondoo. Akaniambia, Maneno haya ni maneno ya kweli ya Mungu.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 100 (K) Ufu. 19:9
(K) Heri walioalikwa karamu ya arusi ya Mwanakondoo.
Mfanyieni Bwana shangwe, dunia yote,
Mtumikieni Bwana kwa furaha;
Njoni mbele zake kwa kuimba. (K)
Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu;
Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake;
Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake. (K)
Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru;
Nyuani mwake kwa kusifu;
Mshukuruni, lihimidini jina lake. (K)
Kwa kuwa Bwana ndiye mwema;
Rehema zake ni za milele;
Na uaminifu wake vizazi na vizazi. (K)
SHANGILIO
Zab. 25:4 , 5
Aleluya, aleluya,
Ee Bwana, unijulishe njia zako, unifundishe mapito yako.
Aleluya.
INJILI
Lk. 21:20-28
Yesu aliwaambia wanafunzi wake: Hapo mtakapoona mji wa
Yerusalemu umezungukwa na majeshi, ndipo jueni ya kwamba uharibifu wake
umekaribia. Ndipo walio katika Uyahudi na wakimbilie milimani, na walio
katikati yake wakimbilie nje, na walio katika mashamba wasiuingie. Kwa kuwa
siku hizo ndizo za mapitilizo, ili yatimizwe yote yaliyoandikwa. Ole wao wenye
miamba na wanaonyonyesha katika siku hizo!
Kwa kuwa kutakuwa na shida katika nchi, na hasira juu ya
taifa hili. Wataanguka kwa ukali wa upanga, nao watatekwa nyara na kuchukuliwa
katika mataifa yote; na Yerusalemu utakanyagwa na Mataifa, hata majira ya
Mataifa yatakapotimia.
Tena, kutakuwa na ishara katika jua; na mwenye, na nyota;
na katika nchi dhiki ya mataifa wakishangaa kwa uvumi wa bahari na msukosuko
wake; watu wakivunjika mioyo kwa hofu, na kwa kutazama mambo yatakayoupata
ulimwengu. Kwa kuwa nguvu z ambinguni zitatikisika. Hapo ndipo watakapomwona
Mwana wa Adamu akija katika wingu pamoja na nguvu na utukufu mwingi. Basi mambo
hayo yaanzapo kutokea, changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi
wenu umekaribia.
Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.
Copyright © 1993 T.M.P. Book Department, Tabora - Tanzania: see MASOMO YA
MISA. Scripture readings from ‘Biblia Takatifu’are published and copyright ©
1975, 1993 by T.M.P. Book Department, Tabora – Tanzania.© Bible Society of
Kenya, © Bible Society of Tanzania.These readings are a reproduction by Furaha
ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment