
“ASALI
ITOKAYO MWAMBANI”
Jumanne,
Oktoba 7, 2025
Juma la
27 la Mwaka wa Kanisa
Kumbukumbu
ya Bikira Maria wa Rozari
Yon 3: 1-10
Zab 130: 1-4, 7-8 (K) 3;
Lk 10: 38-42.
ROZARI:
TAFAKARI NA SALA ILIOJIKITA KATIKA KRISTO !
Wengi
wetu tunasali rozari wenyewe, katika jumuiya au katika familia lakini huenda
mara nyingi hatujui maana yake na umuhimu wake. Mt. Papa Yohane Paulo wa pili
katika barua yake ya Kitume “Rozari ya Bikira Maria” anasema “Rozari, ingawaje
ina tabia ya Maria, katika moyo wake ni sala iliojikita katika Kristo. Ina kina
cha ujumbe wa Injili katika hali yake yote. Ina sauti ya Maria, wimbo wake wa
daima kwa kazi ya ukombozi-umwilisho ilioanza ndani ya tumbo lake…..”.
Kielelezo cha Rosari ni juu ya Yesu-kuzaliwa kwake, maisha yake, kifo na
ufufuko. Sala ya ‘Baba Yetu’ inatukumbusha kwamba Baba yake Yesu ndiye chanzo
cha Ukombozi. ‘Salamu Maria’ inatusaidia kuungana na Maria kutafakari mafumbo
hayo. Inatusaidia kutambua pia Maria alikuwepo na ameunganika na Mwanae katika
mafumbo yote duniani na uwepo wake Mbinguni. ‘Atukuzwe Baba’ inatukumbusha kwamba umuhimu wa maisha yote
ni kwa ajili ya utukufu wa Utatu Mtakatifu. Hivyo, Rozari inatusaidia
kutafakari juu ya umuhimu wa mafumbo ya wokovu wetu.
Rosari
inapaswa ituguse sisi. Ni rahisi. Kurudia kwa maneno kila mara inatusaidia
kujenga hali ambayo tutatafakari mafumbo ya Mungu. Tutambue kuwa, Yesu na Maria
wapo nasi katika furaha na uchungu katika maisha yetu. Tumuombe Bikira Maria
atuombee tuweze kujenga tabia ya ndani ya kusali rosari kila siku. Hii ni
nyenzo ya sala zetu zote: tufikie mahali ambapo “tutasali bila kuchoka” kama
Mtakatifu Paulo alivyosema.
Leo tutasikia nabii Yona ambaye anawahubiria watu wa Ninawi juu ya kuangamizwa kwao kwasababu ya dhambi zao. Lakini pia tunasikia juu ya Mungu, kama Mungu kweli alikuwa ameamua kweli kuwaangamiza si asinge mwambia Yona aende? Ukweli unaweza kuona kwamba Mungu ana huruma kweli kweli, alipenda watubu wapate kuishi! Lakini pia Yona kukataa kwake kuongea kwa niaba ya Mungu pengine Mungu angemuangamiza lakini bado alimuonesha huruma. Mungu ni mwingi wa huruma si mwepesi wa hasira. Bwana kama ungehesabu maovu yetu, nani angesimama? (Zab 130:1). Watu wa Ninawi walifanya uamuzi sahihi kwa kubadili njia zao. Mungu aliona juhudi zao akawakomboa.
Wakati Yesu alivyo watembelea Martha na Maria, Martha alikuwa akijishughulisha jikoni na pale Maria anakaa karibu na miguu ya Yesu huku akimsikiliza akiongea. Martha anamuomba Yesu amwambie Maria amsaidie. Yesu anamwambia Martha ana hofu na mambo mengi, wakati Maria amechagua njia sahihi zaidi. Tunaweza kushangaa kwani Martha hakuwa anafanya jambo lilo sahihi ambalo angepaswa kufanya?
Katika maisha yetu ya kila siku pia, mara nyingi tunafanya kazi tena na tena na wakati mwingine tunasahau kwanini kumekuwa na muda maalumu wa kazi. Watu wa ndoa wake kwa waume, wanapoteza muda mwingi katika kazi, na kuwa na muda kidogo tena sana wakuwa pamoja wao kwa wao na pia kuwa na watoto wao. Mapadre na wale wa maisha ya wakfu, hujikuta wanakuwa na muda mwingi wa kufanya utume na kazi nyingi na hata kuwa na muda mchache wakuwa pamoja na kwasababu ya kuchoka huenda kuacha kusali. Na hii huaribu maisha ya jumuiya kwasababu muda wa kupanga mambo pamoja hukosekana.
Sala:
Ee Bikira Maria, niombee ili kusali rozari kila siku iwe tabia yangu, katika
harakati ya shughuli zangu mbali mbali, muunganiko wa umoja katika matendo
yangu, tabia ya muunganiko mtakatifu, kiburudisho kamili, hali ya kutia moyo
ili kutembea kwa furaha katika njia ya majukumu yangu. Amina
Copyright
©2013-2025 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com
No comments:
Post a Comment