Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

ROZARI: TAFAKARI NA SALA ILIOJIKITA KATIKA KRISTO !



 “ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumatatu, Oktoba 7, 2024
Juma la 27 la Mwaka wa Kanisa

Kumbukumbu ya Bikira Maria wa Rozari

Gal 1: 6-12 
Zab 111: 1-2, 7-10 
Lk 10: 27-37


ROZARI: TAFAKARI NA SALA ILIOJIKITA KATIKA KRISTO !


Wengi wetu tunasali rozari wenyewe, katika jumuiya au katika familia lakini huenda mara nyingi hatujui maana yake na umuhimu wake. Mt. Papa Yohane Paulo wa pili katika barua yake ya Kitume “Rozari ya Bikira Maria” anasema “Rozari, ingawaje ina tabia ya Maria, katika moyo wake ni sala iliojikita katika Kristo. Ina kina cha ujumbe wa Injili katika hali yake yote. Ina sauti ya Maria, wimbo wake wa daima kwa kazi ya ukombozi-umwilisho ilioanza ndani ya tumbo lake…..”. Kielelezo cha Rosari ni juu ya Yesu-kuzaliwa kwake, maisha yake, kifo na ufufuko. Sala ya ‘Baba Yetu’ inatukumbusha kwamba Baba yake Yesu ndiye chanzo cha Ukombozi. ‘Salamu Maria’ inatusaidia kuungana na Maria kutafakari mafumbo hayo. Inatusaidia kutambua pia Maria alikuwepo na ameunganika na Mwanae katika mafumbo yote duniani na uwepo wake Mbinguni. ‘Atukuzwe Baba’  inatukumbusha kwamba umuhimu wa maisha yote ni kwa ajili ya utukufu wa Utatu Mtakatifu. Hivyo, Rozari inatusaidia kutafakari juu ya umuhimu wa mafumbo ya wokovu wetu.

Rosari inapaswa ituguse sisi. Ni rahisi. Kurudia kwa maneno kila mara inatusaidia kujenga hali ambayo tutatafakari mafumbo ya Mungu. Tutambue kuwa, Yesu na Maria wapo nasi katika furaha na uchungu katika maisha yetu. Tumuombe Bikira Maria atuombee tuweze kujenga tabia ya ndani ya kusali rosari kila siku. Hii ni nyenzo ya sala zetu zote: tufikie mahali ambapo “tutasali bila kuchoka” kama Mtakatifu Paulo alivyosema.

Leo katika Injili mwalimu wa sheria anamuuliza Yesu swali ambalo, sisi tungeweza kujiuliza katika maisha yetu ya kila siku. “Bwana, nifanye nini niurithi Ufalme wa milele?” (Lk 10: 25). Yesu, lakini, tena katika hekima anajibu kwa yale yalioandikwa katika Maandiko: ‘kumpenda Bwana Mungu wako na jirani yako kama nafsi yako’ (rej. Lk 10: 27). Kupenda maana yake ni kujitoa kwa wengine kwa yote tulio nayo na yote jinsi tulivyo. 

Kujitoa kusikiliza wengine kujitoa kuelewa wengine na kuwa na subira kwa ajili ya wengine. Huo ndio upendo. Upendo huu unakuwa na asili ya Kimungu tunapo ueneza zaidi kwa wale walio tuumiza katika maisha au kwa wengine tusio waona hata macho kwa macho. Upendo unakuwa na Mguso wa Kimungu tunapo toka njee kwenda kuwasaidia hata watu tusio wafahamu. ‘Kama mtu mmoja anateseka, watu wote wanateseka naye, kama mmoja anaheshimiwa, watu wote wanashiriki katika furaha yake’ (1 Kor 12: 26). Hii ndio fadhila ya Msamaria Mwema. 

Sala: Ee Bikira Maria, niombee ili kusali rozari kila siku iwe tabia yangu, katika harakati ya shughuli zangu mbali mbali, muunganiko wa umoja katika matendo yangu, tabia ya muunganiko mtakatifu, kiburudisho kamili, hali ya kutia moyo ili kutembea kwa furaha katika njia ya majukumu yangu. Amina


Copyright ©2013-2024 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

No comments:

Post a Comment