Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

KUMWELEKEA YESU!


“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumanne, Oktoba 8, 2024 
Juma la 27 la Mwaka


Gal 1:13-24; 
Zab 139: 1-3, 13-15;
Lk 10: 38-42.


KUMWELEKEA YESU!

Wakati Yesu alivyo watembelea Martha na Maria, Martha alikuwa akijishughulisha jikoni na pale Maria anakaa karibu na miguu ya Yesu huku akimsikiliza akiongea. Martha anamuomba Yesu amwambie Maria amsaidie. Yesu anamwambia Martha ana hofu na mambo mengi, wakati Maria amechagua njia sahihi zaidi. Tunaweza kushangaa kwani Martha hakuwa anafanya jambo lilo sahihi ambalo angepaswa kufanya? 

Katika maisha yetu ya kila siku pia, mara nyingi tunafanya kazi tena na tena na wakati mwingine tunasahau kwanini kumekuwa na muda maalumu wa kazi. Watu wa ndoa wake kwa waume, wanapoteza muda mwingi katika kazi, na kuwa na muda kidogo tena sana wakuwa pamoja wao kwa wao na pia kuwa na watoto wao. Mapadre na wale wa maisha ya wakfu, hujikuta wanakuwa na muda mwingi wa kufanya utume na kazi nyingi na hata kuwa na muda mchache wakuwa pamoja na kwasababu ya kuchoka huenda kuacha kusali. Na hii huaribu maisha ya jumuiya kwa sababu muda wa kupanga mambo pamoja hukosekana. 

Katika Injili Maria anachukua nafasi sahihi kwa kuchagua kubaki na Yesu. Na hapa tunaona matokeo ya uchaguzi wa mtu binafsi. Uchaguzi wa mtu unampa uzima wa milele au kifo na uharibifu. Kila mmoja wetu anaitwa kufanya uchaguzi sahihi kwa maisha yake. Mfanye Mungu rafiki yako na utafurahia urafiki wake milele.

Sala: Ee Bwana nichague wewe uliye njia sahihi. Amina


Copyright ©2013-2024 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com.

No comments:

Post a Comment