“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumatano,
Oktoba 16, 2024
Juma
la 28 la Mwaka wa Kanisa
Gal
5:18-25;
Zab
1:1-4, 6;
Lk
11:42-46
KUJIZOESHA
KUTENDA FADHILA!
Katika
somo la kwanza leo Mt. Paulo leo anaorodhesha baadhi ya vitu ambavyo Wagalatia
wanapaswa kuepuka. Anasema kuna baadhi ya matendo ya mwili. Pengine ni kama
tunavyosikia baadhi yake ni, mumonyoko wa maadili, uasherati, kuabudu miungu
mingine, ushirikina, ulevi na anasa, tunaweza kujisifia na kusema, Oh! Mimi
sitendi kati ya hayo. Hii inaweza kutufanya turidhike na kujiona bora kuliko
wengine. Lakini hata hivyo, tukipitia hiyo orodha kwa makini na kwa ndani
kabisa, tunaweza kutambua kwa namna moja au nyingine tunahitaji Roho wa Mungu
zaidi ili tuweze kuwa wema na kuepuka hayo.
Yesu
anawataja walimu washeria na Mafarisayo kwa maneno makali kabisa. Yesu anatumia
mfano wa zaka kuonesha ni kwa jinsi ghani walivyotoka njee ya mstari. Mungu
alitaka sadaka ya mazao ya kwanza kama shukrani na heshima ya nguvu zake kwa
kujali watu wake (Kumb. 14: 22; Lev. 27: 30).
Waandishi
walienda mbali zaidi na kuwatoza watu zaidi tena kwa kutumia mahesabu na ujazo
usio wa muhimu, na kushindwa kuwajali maskini na wahitaji. Walishikwa na wivu
na kushindwa kuwapenda wengine. Yesu pia anawalinganisha pia na “makaburi yasio
na mipaka” ilikuwa mtu akijigusa na kaburi alikuwa anatiwa najisi kwa muda wa
siku saba (Hes 19:16). Wale wote waliokuja kuwasikiliza Mafarisayo na waandishi
kadhalika walitiwa unajisi kwa mafundisho yao ya uongo.
Kiini
cha amri za Mungu ni upendo. Mungu ni Upendo na kila kitu anchotenda kinatoka
katika upendo wake kwetu sisi. Je, una ruhusu Upendo wa Mungu ubadili akili
yako na moyo wako? Je, upo tayari kukuwa katika fadhila katika upendo kwa Mungu
na jirani? Fadhila inapaswa kupaliliwa kwa sala na matendo mema ili zikuwe na
zimee ndani kabisa mwa mioyo yetu, ili ziweze kukomaa na kuchanua. Kama vile
mimea inavyo hitaji maji na mbolea ili imee vizuri, ndivyo na fadhila za
Kimungu zinapaswa kumwagiliwa kwa kuzitenda kila wakati na kuwa karibu zaidi na
Mungu. Tumuombe Mungu atusaidie kusogea
karibu naye daima, kadiri unavyokuwa karibu na taa ndivyo uhakika wakuona
unakuwepo. usaidie kusogea karibu naye daima, kadiri unavyokuwa karibu na taa
ndivyo uhakika wakuona unakuwepo. Tuishi kama Mungu anavyopenda ili tutende kwa
upendo kama Mungu anavyotutendea.
Sala:
Bwana, washa ndani ya moyo wangu kwa upendo ili niweze kutenda yale yalio ya
lazima kabisa-Upendo kwa Mungu na Upendo kwa Jirani. Amina.
Copyright
©2013-2024 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com
No comments:
Post a Comment