Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

KUFAFANUA ALAMA ZA NYAKATI ZETU!




























 “ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Ijumaa, Oktoba, 21, 2022
Juma la 29 la Mwaka wa Kanisa

Ef 4:1-6;
Zab 23:1-6;
Lk 12:54-59


KUFAFANUA ALAMA ZA NYAKATI ZETU!

Injili ya leo kutoka kwa Mt. Luka, inatuelezea ni kwa jinsi ghani watu wakipindi cha Yesu walivyokuwa wakiweza kufafanua majira na nyakati zao, kutambua uso wa nchi na mbingu, lakini walishindwa kutambua alama za Yesu alizoweka mbele ya macho yao katika kutangaza Ufalme wa Mungu. Je, si kweli zaidi hata kwetu sasa? Tumebobea sana katika teknologia na tunajivuna katika hali ya ukuwaji wa sayansi tuliofanya kama jamii, lakini mara nyingi tunakosa ujumbe wa Mungu anaojaribu kuwasiliana nasi kila siku.

“Alama za nyakati” ilikuwa ni ujumbe muhimu katika mkutano wa pili wa Vatikan, kama ulivyotutaka kuelezea ujumbe wa Mungu katika alama za nyakati zetu, na pia kubaki katika ukweli wa ujumbe wa Yesu na habari njema iliohubiriwa na Mababa wa kanisa. Wakati watu wanaongelea kuhusu siasa, michezo au dini, mara nyingi midahalo ni ya kutumia nguvu nyingi na hisia. Lakini tunapoulizwa ni nini mpango wa Mungu katika maisha yetu, wengi wetu twaweza kusema hatujui. Mara nyingi hatuna uhakika na anacho tuambia Mungu tufanye katika maisha yetu, tofauti na mipango yetu na tamaa zetu. Mara nyingi tunajifanya na kupotea huku tukijifanya hamna chochote kibaya kwa uchaguzi wetu na maamuzi yetu; kwa kifupi, inatuwia vigumu kubadilika. Mt. Paulo katika somo la kwanza anawaandikia Waefeso akiwaeleza kuwa wajiandae kushika mambo ya msingi kwa kushika njia sahihi. Waenende kadiri ya wito wao walioitiwa na Mungu.

Sala: Bwana, tusaidie leo, ili tuweze kuelezea kwa usahihi neno lako kwa njia ya alama za nyakati zetu. Amina


Copyright ©2013-2022 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

No comments:

Post a Comment