“ASALI
ITOKAYO MWAMBANI”
Jumamosi,
Oktoba 12, 2024
Juma la
27 la Mwaka wa Kanisa
Gal 3:
22-29;
Zab
104: 2-7;
Lk 11:
27-28
KUBADILI
MAVAZI!
Somo la
kwanza linatukumbusha sisi, Wakristo wabatizwa, kwamba katika ubatizo
tulivalishwa vazi ambalo ni Kristo. Imani katika Kristo ilitubatiza ‘ndani ya
Kristo’. Ubatizo huu wa Roho unamtambulisha mwamini na Kristo na unamfanya awe
sehemu ya mwili wa Kristo. Ubatizo kwa njia ya maji ni ishara ya njee ya hii
kazi ya ndani ya Roho Mtakatifu. Mwamini anapaswa atupilie mbali mavazi ya
dhambi na kwa Imani, apokee mshipi na mavazi mapya ya haki yakumfunga ndani
Kristo. Injili ya leo inauhusiano na Lk 8: 19-21, ambapo inaongelea kuhusu Mama
na ndugu wa Yesu walitaka kumuona, inatoa somo lilelile kwamba mahusiano ya njee
si zaidi ya kusikia neno la Mungu na kulitii.
Kwa Injili ya Luka, Maria
amebarikiwa kuliko wanawake wote. Lakini pia amebarikiwa kuliko wanawake wote
si kwasababu ya kumzaa Mwana wa Mungu tu bali ni kwasababu aliliamini neno la
Mungu na kulishika. Kwahiyo Yesu alivyosema wana heri zaidi wanao lishika neno
la Mungu na kulitenda, Maria ni wakwanza kabisa tena kwa uaminifu mkubwa
kulishika Neno la Mungu na kulitenda, hivyo Yesu haku maanisha kumtenga au
kumkataa Mama yake. Wale wote wanaolisikia Neno la Mungu na kulitenda
wanabarikiwa. Bikira Maria alivaa vazi la Imani isio yumba yumba na
alijikabidhi kwa Mungu.
Kama
isivyowezekana kulitenga Kanisa na Kristo, ndivyo isivyowezekana kumtenga Maria
na Yesu. Yeye ni mfano unaongara katika kulishika Neno la Mungu. Maria
anatufundisha jinsi ya kukubali na kulishika Neno la Mungu, jinsi ya kuliweka
katika ubinadamu wetu, kuliishi, kuliweka ndani, nakulifanya lizae matunda
mema. Kulifanya likue, na kuchukua sura mpya ndani mwetu, hata wakati tusipo
lielewa au wakati linatufanya tuteseke. Wana heri wanaosikia Neno la Mungu na
kulishika.
Sala:
Bwana, tusaidie tuweze kuvaa vazi jipya la Upendo, huruma, haki na usawa. Amina
Copyright
©2013-2024 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com
No comments:
Post a Comment