Everyday Saint / Maisha ya Watakatifu

IMANI ILIYO JARIBIWA!



“ASALI ITOKAYO MWAMBANI”
Jumamosi, Oktoba 19, 2024
Juma la 28 la Mwaka



Efe 1: 15-23;
Zab 8: 2-7; 
Lk 12: 8-12.


IMANI ILIYO JARIBIWA!

Nguvu na uwezo unajaribiwa zaidi ya kuwa na vyeti. Hii ni kweli pia katika Imani yetu. Sio wengi watakao simama katika kujaribiwa huku kwa Imani. Yesu analifahamu hili na anataka kutoa somo kamili katika Injili. Masharti yake kama vile, ‘Kama” “Lakini” yanamuonesha wito wake kwetu wa kuwa makini. Haongei kwa mafumbo wala mfano. Anataka Imani kamili isiotikiswa kwa Mungu na msukumo kamili katika kumfuata Yeye katika hali zote. 

Kukubali kwamba wewe ni Mkristo kwa baadhi ya Nchi inamaana umejitangazia kifo. Na sehemu nyingine, ina maana umejitangazia, mateso, kukataliwa baadhi ya huduma au kuto kuchaguliwa kwa ajili ya jambo flani. Ni katika hali hiyo pia kumkubali Kristo inaweza kuhatarisha mambo binafsi, usalama wako wa kifedha na umuhimu wako pengine. Lakini Yesu anasisitisa kwamba kama tunataka kukubaliwa mbinguni mbele ya Malaika watakatifu kama watoto wa kweli wa Mungu, tunapaswa kukiri ukweli huo mbele ya ulimwengu, hata katika mateso na kutengwa. 

Kanisa lina wakumbuka watakatifu kwa sababu hii. Utukufu wao ni matokeo ya Imani yao na kujitoa kwao katika maisha yao ya Ukristo. Mt. Teresia wa Avila ambaye tunamkumbuka leo ni mmoja wapo katika hili. Mwanamke aliyekuwa na Imani ya juu kabisa, alipighana na mambo yote yaliokuwa kinyume wakati wake ili kuleta mabadiliko katika shirika la Wakarmeli. Maisha ya sala yalikuwa ndio silaha yake kuu, na zaidi ya yote Yesu aliyesema “ msiwe na wasi wasi mtasema nini” kila mara alisimama kadiri ya Imani yake. Huu ndio wito wetu kuwa imara katika kila hali.

Sala: “Kusiwe na kitu cha kukusumbua. Kila kitu kitapita. Mungu habadiliki. Uvumilivu unapata mambo yote. Hahitaji kitu mtu aliye na Mungu. Mungu mwenyewe anatenda”. Amina.


Copyright ©2013-2024 ©FurKat, Furaha ya Kikatoliki: see www.fur-kat.blogspot.com

No comments:

Post a Comment